Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Luka 23:43 - Swahili Revised Union Version

Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Yesu akamjibu, “Nakuambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Yesu akamjibu, “Nakuambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Yesu akamjibu, “Nakuambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Isa akamjibu, “Amin, nakuambia, leo utakuwa pamoja nami Paradiso.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Isa akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Luka 23:43
22 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo nikakuungamia dhambi yangu, Wala sikuuficha upotovu wangu. Nilisema, Nitayakiri maasi yangu kwa BWANA, Nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.


Uniite siku ya mateso; Nitakuokoa, nawe utanitukuza.


Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki Atawafanya wengi kuwa wenye haki; Naye atayachukua maovu yao.


Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa bado wanena, nitasikia.


Ni nani aliye Mungu kama wewe, mwenye kusamehe uovu, na kuliachilia kosa la watu wa urithi wake waliosalia? Hadumishi hasira yake milele, kwa maana yeye hufurahia rehema.


Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.


Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.


Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi muwepo.


Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami popote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu.


Lakini tuna moyo mkuu; nasi tunaona ni afadhali kutokuwemo katika mwili na kukaa pamoja na Bwana.


Ninasongwa katikati ya mambo mawili; ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo maana ni vizuri zaidi sana;


Naye, kwa sababu hii, anaweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.


Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho anayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu.