Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Luka 21:19 - Swahili Revised Union Version

Nanyi kwa subira yenu mtaziponya nafsi zenu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nanyi kwa subira yenu mtaziponya nafsi zenu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Luka 21:19
26 Marejeleo ya Msalaba  

Utulie mbele za BWANA, Nawe umngojee kwa subira; Usihangaike juu ya afanikiwaye katika njia yake, Wala mtu apangaye maovu.


Nilimngoja BWANA kwa subira, Akaniinamia na kusikia kilio changu.


Nikasikia, na tumbo langu likatetemeka, Midomo yangu ikatikisika kwa sauti ile; Ubovu ukaingia mifupani mwangu, Nikatetemeka katika mahali pangu; Ili nipate kuingoja ile siku ya dhiki, Kundi lao washambuliao wakweapo juu ya watu.


Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.


Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.


Na zile penye udongo mzuri, ndio wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno, na kulishika; kisha huzaa matunda kwa kuvumilia.


Kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi; ili kwa saburi na faraja ya Maandiko tupate kuwa na tumaini.


wale ambao kwa subira katika kutenda mema wanatafuta utukufu na heshima na kutoharibika, watapewa uzima wa milele;


Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta subira;


na kazi ya subira ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;


Bali tukikitumainia kitu tusichokiona, twakingojea kwa subira.


Wala hatuachi kuikumbuka kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya upendo, na subira yenu ya tumaini lililo katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele za Mungu Baba yetu.


Bwana awaongoze mioyo yenu mkapate pendo la Mungu, na subira ya Kristo.


Maana mnahitaji saburi, ili kwamba mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu mpate ile ahadi.


Nasi twataka sana kila mmoja wenu aidhihirishe bidii ile ile, kwa utimilifu wa matumaini hata mwisho;


Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi.


mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.


Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno.


na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu subira, na katika subira yenu utauwa,


Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya Yesu Kristo, nilikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu.


Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye subira na imani ya watakatifu.


Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu.


Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi.