Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 32:3 - Swahili Revised Union Version

Tena macho yao waonao hayatakuwa na kiwi, na masikio yao wasikiao yatasikiliza.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Macho hayatafumbwa tena, masikio yatabaki wazi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Macho hayatafumbwa tena, masikio yatabaki wazi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Macho hayatafumbwa tena, masikio yatabaki wazi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ndipo macho ya wale wanaoona hayatafumbwa tena, nayo masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ndipo macho ya wale wanaoona hayatafumbwa tena, nayo masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Tena macho yao waonao hayatakuwa na kiwi, na masikio yao wasikiao yatasikiliza.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 32:3
14 Marejeleo ya Msalaba  

Na katika siku hiyo viziwi watasikia maneno ya hicho kitabu, na macho ya vipofu yataona katika upofu na katika giza.


Hao nao wakosao rohoni mwao watapata kufahamu, na hao wanung'unikao watakubali mafunzo.


Na tena nuru ya mwezi itakuwa kama nuru ya jua, na nuru ya jua itaongezeka mara saba, kama nuru ya siku saba, katika siku ile BWANA atakapofunga mapigo ya watu wake, na kuliponya pigo la jeraha lao.


Nitawaleta vipofu kwa njia wasiyoijua; katika mapito wasiyoyajua nitawaongoza; nitafanya giza kuwa nuru mbele yao; na mahali palipopotoka kuwa pamenyoka. Haya nitayatenda, wala sitawaacha.


Na watoto wako wote watafundishwa na BWANA; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi.


Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue BWANA; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hadi aliye mkubwa miongoni mwao, asema BWANA; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena.


Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa.


wakashangaa mno kupita kiasi, wakinena, Ametenda mambo yote vema; viziwi awafanya wasikie, na bubu waseme.


uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi.


Kwa kuwa Mungu, aliyesema, Nuru itang'aa toka gizani, ndiye aliyeng'aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo.