Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 2:7 - Swahili Revised Union Version

Tena nchi yao imejaa fedha na dhahabu, wala hapana mwisho wa hazina zao; tena nchi yao imejaa farasi, wala hapana mwisho wa magari yao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nchi yao imejaa fedha na dhahabu, hazina yao ni kubwa kupindukia. Nchi yao imejaa farasi, magari yao ya kukokotwa hayana idadi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nchi yao imejaa fedha na dhahabu, hazina yao ni kubwa kupindukia. Nchi yao imejaa farasi, magari yao ya kukokotwa hayana idadi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nchi yao imejaa fedha na dhahabu, hazina yao ni kubwa kupindukia. Nchi yao imejaa farasi, magari yao ya kukokotwa hayana idadi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nchi yao imejaa fedha na dhahabu, hakuna mwisho wa hazina zao. Nchi yao imejaa farasi, hakuna mwisho wa magari yao ya vita.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nchi yao imejaa fedha na dhahabu, hakuna mwisho wa hazina zao. Nchi yao imejaa farasi, hakuna mwisho wa magari yao.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Tena nchi yao imejaa fedha na dhahabu, wala hapana mwisho wa hazina zao; tena nchi yao imejaa farasi, wala hapana mwisho wa magari yao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 2:7
15 Marejeleo ya Msalaba  

Tena Sulemani alikuwa na mabanda ya farasi elfu arubaini kwa magari yake, na wapandao farasi elfu kumi na mbili.


Au pamoja na wakuu wenye dhahabu, Waliozijaza nyumba zao fedha;


Hawa wanataja magari na hawa farasi, Lakini sisi tutalitaja jina la BWANA, Mungu wetu.


Bali ninyi mlisema, La! Maana tutakimbia juu ya farasi; basi, ni kweli, mtakimbia; tena, Sisi tutakimbia juu ya wanyama waendao upesi; basi, wale watakaowafuatia watakuwa wepesi.


Ole wao wateremkao kwenda Misri wapate msaada, na kutegemea farasi; watumainio magari kwa kuwa ni mengi, na wapanda farasi kwa kuwa ni hodari sana; lakini hawamwangalii Mtakatifu wa Israeli, wala hawamtafuti BWANA!


Kwa sababu ya uovu wa kutamani kwake niliona hasira, nikampiga; nilificha uso wangu, nikaona ghadhabu; naye akaendelea kwa ukaidi, kuifuata njia ya moyo wake mwenyewe.


Ashuru hatatuokoa; hatutapanda farasi; wala hatutaiambia tena kazi ya mikono yetu, Ninyi ndinyi miungu yetu; maana kwako wewe wasio na baba hupata rehema.


Kisha itakuwa katika siku hiyo, asema BWANA, nitawakatilia mbali farasi wako watoke kati yako, nami nitayaharibu magari yako ya vita;


kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake.