Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Hosea 10:7 - Swahili Revised Union Version

Katika habari za Samaria, mfalme wake amekatiliwa mbali, kama povu usoni pa maji.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mfalme wa Samaria atachukuliwa, kama kipande cha mti juu ya maji.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mfalme wa Samaria atachukuliwa, kama kipande cha mti juu ya maji.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mfalme wa Samaria atachukuliwa, kama kipande cha mti juu ya maji.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya maji.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya uso wa maji.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Katika habari za Samaria, mfalme wake amekatiliwa mbali, kama povu usoni pa maji.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Hosea 10:7
9 Marejeleo ya Msalaba  

Ikawa baada ya hayo, Nabothi Myezreeli alikuwa na shamba la mizabibu katika Yezreeli, karibu na nyumba ya kifalme ya Ahabu mfalme wa Samaria.


Lakini malaika wa BWANA akamwambia Eliya Mtishbi, Ondoka, uende ukaonane na wale wajumbe wa mfalme wa Samaria, ukawaambie, Je! Ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli, hata mnakwenda kuuliza kwa Baal-zebubu, mungu wa Ekroni?


Na Hoshea mwana wa Ela akamfitinia Peka mwana wa Remalia, akampiga, akamwua, akatawala mahali pake, katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.


Mfalme wa Ashuru akaona fitina katika huyo Hoshea; kwa maana alikuwa ametuma wajumbe kwa So, mfalme wa Misri, wala hakumletea kodi mfalme wa Ashuru, kama alivyofanya mwaka kwa mwaka; kwa hiyo mfalme wa Ashuru akamfunga, akamtia kifungoni.


Hivyo ndivyo Betheli atakavyowatenda ninyi, kwa sababu ya ubaya wenu mwingi; wakati wa mapambazuko mfalme wa Israeli atakatiliwa mbali kabisa.


Yakini sasa watasema, Hatuna mfalme; kwa maana hatumchi BWANA; na mfalme huyu je! Aweza kututendea nini?


Mahali pa Aveni palipoinuka, yaani, dhambi ya Israeli, pataharibika; mwiba na mbigili itamea juu ya madhabahu zake; nao wataiambia milima, Tusitirini; na vilima, Tuangukieni.


Nimekupa mfalme katika hasira yangu, nikamwondoa katika ghadhabu yangu.


ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele.