Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Danieli 6:17 - Swahili Revised Union Version

Likaletwa jiwe, likawekwa mdomoni mwa lile tundu; naye mfalme akalitia mhuri kwa mhuri wake mwenyewe, na kwa mhuri wa wakuu wake, lisibadilike neno lolote katika habari za Danieli.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Jiwe likaletwa na kuwekwa mlangoni mwa lile pango. Mfalme akalipiga mhuri wake binafsi na ule wa wakuu wake, ili uamuzi kuhusu Danieli usibatilishwe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Jiwe likaletwa na kuwekwa mlangoni mwa lile pango. Mfalme akalipiga mhuri wake binafsi na ule wa wakuu wake, ili uamuzi kuhusu Danieli usibatilishwe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Jiwe likaletwa na kuwekwa mlangoni mwa lile pango. Mfalme akalipiga mhuri wake binafsi na ule wa wakuu wake, ili uamuzi kuhusu Danieli usibatilishwe.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mlango wa tundu, naye mfalme akalitia muhuri kwa pete yake mwenyewe pamoja na kwa pete za wakuu wake, ili hali ya Danieli isiweze kubadilishwa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mdomo wa tundu, naye mfalme akalitia muhuri kwa pete yake mwenyewe pamoja na kwa pete za wakuu wake, ili hali ya Danieli isiweze kubadilishwa.

Tazama sura

Swahili Roehl Bible 1937

Pakaletwa jiwe moja, likawekwa juu hapo pa kuliingilia lile pango, mfalme akalitia muhuri kwa pete yake yenye muhuri na kwa pete ya wakuu wake yenye muhuri, jambo la Danieli lisigeuzwe.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Danieli 6:17
7 Marejeleo ya Msalaba  

Yeye atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.


Naye mfalme Sedekia akasema, Tazama, yuko mikononi mwenu; maana mfalme siye awezaye kufanya neno lolote kinyume chenu.


Wameukatilia mbali uhai wangu gerezani, Na kutupa jiwe juu yangu.


Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu.


akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia mhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe kwa muda mfupi.