Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Danieli 11:43 - Swahili Revised Union Version

Lakini atakuwa na nguvu juu ya hazina za dhahabu na fedha, na juu ya vitu vyote vya Misri vyenye thamani; na Walibya na Wakushi watafuata nyayo zake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na vito vyote vya thamani vya nchi ya Misri. Watu wa Libia na watu wa Kushi watafuata nyayo zake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na vito vyote vya thamani vya nchi ya Misri. Watu wa Libia na watu wa Kushi watafuata nyayo zake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na vito vyote vya thamani vya nchi ya Misri. Watu wa Libia na watu wa Kushi watafuata nyayo zake.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Atamiliki hazina za dhahabu na fedha na utajiri wote wa Misri, huku Walibia na Wakushi wakijisalimisha kwake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha.

Tazama sura

Swahili Roehl Bible 1937

Namo mikononi mwake mwenye nguvu vitakuwamo vilimbiko vya dhahabu na vya fedha na vyombo vyote vya Misri vipendezavyo; kwa hiyo nao Walibia na Wanubi watamfuata.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Danieli 11:43
9 Marejeleo ya Msalaba  

akiwa na magari elfu moja na mia mbili, na wapanda farasi elfu sitini; na watu wasiohesabika, waliotoka Misri pamoja naye; Walubi, na Wasukii, na Wakushi.


Tena hao watumishi wako wote wataniteremkia kwangu mimi, nao watanisujudia, wakisema, Toka wewe, na hawa watu wote wakufuatao; na baada ya hayo nitatoka. Basi akatoka kwa Farao na hasira kuu.


Uajemi, na Kushi, na Putu, pamoja nao; wote wana ngao na chapeo;


Naye ataunyosha mkono wake juu ya nchi hizo, hata na nchi ya Misri haitaokoka.


Lakini habari zitokazo mashariki na kaskazini zitamfadhaisha; naye atatoka kwa ghadhabu nyingi, ili kuharibu, na kuwaondolea mbali watu wengi.


Kushi na Misri walikuwa nguvu zake, nazo zilikuwa hazina mpaka; Puti na Walibya walikuwa wasaidizi wake.


Baraka akawakutanisha Naftali na Zabuloni waende Kedeshi wakakwea watu elfu kumi wakimfuata; Debora naye akaenda pamoja naye.