Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Amosi 7:6 - Swahili Revised Union Version

BWANA akaghairi katika jambo hili pia. Jambo hili halitakuwa, asema Bwana MUNGU.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Basi, Mwenyezi-Mungu akabadili nia yake, akasema: “Hili pia halitatukia.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Basi, Mwenyezi-Mungu akabadili nia yake, akasema: “Hili pia halitatukia.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Basi, Mwenyezi-Mungu akabadili nia yake, akasema: “Hili pia halitatukia.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa hiyo Mwenyezi Mungu akaghairi. Bwana Mungu Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa hiyo bwana akaghairi. bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

BWANA akaghairi katika jambo hili pia. Jambo hili halitakuwa, asema Bwana MUNGU.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Amosi 7:6
16 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewaumba.


Naye Mungu akatuma malaika aende Yerusalemu ili auangamize; naye alipokuwa tayari kuangamiza, BWANA akatazama, akaghairi katika mabaya, akamwambia malaika aharibuye, Basi yatosha; sasa ulegeze mkono wako. Naye malaika wa BWANA akasimama karibu na kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi.


Akawakumbukia agano lake; Akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake;


Kwa kuwa BWANA atawaamua watu wake, Na kuwahurumia watumishi wake.


Lakini Yeye, kwa kuwa anayo rehema, Husamehe uovu wala haangamizi. Mara nyingi huipishia mbali ghadhabu yake, Wala haiwashi hasira yake yote.


Urudi, Ee BWANA utakasirika hadi lini? Wahurumie watumishi wako.


Na BWANA akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake.


Je! Hezekia, mfalme wa Yuda, na watu wote wa Yuda, walimwua Mikaya? Je! Hakumcha BWANA, na kumwomba BWANA awafadhili; naye BWANA akaghairi, asiyatende mabaya yale aliyoyatamka juu yao? Lakini sisi tuko karibu kujiletea maafa makuu wenyewe.


Ikiwa mtabaki katika nchi hii, ndipo nitawajenga, wala sitawabomoa, nami nitawapanda, wala sitawang'oa; kwa maana nayajutia mabaya niliyowatenda.


rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi kuadhibu.


BWANA akaghairi katika jambo hili. Jambo hili halitakuwa, asema BWANA.


Haya ndiyo aliyonionesha; na tazama, Bwana alisimama karibu na ukuta uliojengwa kwa timazi, mwenye timazi mkononi mwake.


Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende.


Akamwomba BWANA, akasema, Nakuomba, Ee BWANA; sivyo hivyo nilivyosema, hapo nilipokuwa katika nchi yangu? Hii ndiyo sababu nilifanya haraka kukimbilia Tarshishi; kwa maana nilijua ya kuwa wewe u Mungu mwenye neema, umejaa huruma, si mwepesi wa hasira, u mwingi wa rehema, nawe waghairi mabaya.


Nao wakaiondoa hiyo miungu ya kigeni iliyokuwa kati yao, nao wakamtumikia BWANA; na roho yake ilihuzunika kwa sababu ya msiba wa Israeli.


Na kila wakati BWANA alipowainulia waamuzi, ndipo BWANA alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa na mikono ya adui zao siku zote za mwamuzi huyo; maana BWANA alisikitishwa na kilio chao kwa sababu ya watu wale waliowaonea na kuwasumbua.