Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Amosi 7:3 - Swahili Revised Union Version

3 BWANA akaghairi katika jambo hili. Jambo hili halitakuwa, asema BWANA.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Basi, Bwana Mwenyezi-Mungu akabadili nia yake, akasema, “Haitakuwa hivyo!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Basi, Bwana Mwenyezi-Mungu akabadili nia yake, akasema, “Haitakuwa hivyo!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Basi, Bwana Mwenyezi-Mungu akabadili nia yake, akasema, “Haitakuwa hivyo!”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Kwa hiyo Mwenyezi Mungu akaghairi. Kisha Mwenyezi Mungu akasema, “Hili halitatokea.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Kwa hiyo bwana akaghairi. Kisha bwana akasema, “Hili halitatokea.”

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

3 BWANA akaghairi katika jambo hili. Jambo hili halitakuwa, asema BWANA.

Tazama sura Nakili




Amosi 7:3
16 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewaumba.


Naye Mungu akatuma malaika aende Yerusalemu ili auangamize; naye alipokuwa tayari kuangamiza, BWANA akatazama, akaghairi katika mabaya, akamwambia malaika aharibuye, Basi yatosha; sasa ulegeze mkono wako. Naye malaika wa BWANA akasimama karibu na kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi.


Akawakumbukia agano lake; Akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake;


Lakini Yeye, kwa kuwa anayo rehema, Husamehe uovu wala haangamizi. Mara nyingi huipishia mbali ghadhabu yake, Wala haiwashi hasira yake yote.


Urudi, Ee BWANA utakasirika hadi lini? Wahurumie watumishi wako.


Na BWANA akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake.


Je! Hezekia, mfalme wa Yuda, na watu wote wa Yuda, walimwua Mikaya? Je! Hakumcha BWANA, na kumwomba BWANA awafadhili; naye BWANA akaghairi, asiyatende mabaya yale aliyoyatamka juu yao? Lakini sisi tuko karibu kujiletea maafa makuu wenyewe.


Ikiwa mtabaki katika nchi hii, ndipo nitawajenga, wala sitawabomoa, nami nitawapanda, wala sitawang'oa; kwa maana nayajutia mabaya niliyowatenda.


Niwezeje kukuacha, Efraimu? Niwezeje kukuachilia Israeli? Niwezeje kukufanya kama Adma? Niwezeje kukuweka kama Seboimu? Moyo wangu umegeuka ndani yangu, huruma zangu zimewaka pamoja.


rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi kuadhibu.


Ni nani ajuaye kwamba hatarudi na kugeuka, na kutuachia baraka nyuma yake, naam, sadaka ya unga, na sadaka ya kinywaji, kwa BWANA, Mungu wenu?


Yachukieni mabaya; yapendeni mema; mkaithibitishe haki langoni; yamkini kwamba BWANA, Mungu wa majeshi, atawafanyia fadhili mabaki ya Yusufu.


BWANA akaghairi katika jambo hili pia. Jambo hili halitakuwa, asema Bwana MUNGU.


Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende.


Kwa kuwa BWANA atawaamua watu wake, Atawahurumia watumwa wake, Aonapo ya kuwa nguvu zao zimeondoka, Na ya kuwa habaki mtu, aliyefungwa wala asiyefungwa,


Basi ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, ili mpate kuponywa. Sala yake mwenye haki ina nguvu nyingi, na hutenda mengi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo