Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Wafalme 8:12 - Swahili Revised Union Version

Ndipo Sulemani akanena, BWANA alisema ya kwamba atakaa katika giza nene.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ndipo Solomoni akasema, “Mwenyezi-Mungu alisema kwamba, atakaa katika giza nene.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ndipo Solomoni akasema, “Mwenyezi-Mungu alisema kwamba, atakaa katika giza nene.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ndipo Solomoni akasema, “Mwenyezi-Mungu alisema kwamba, atakaa katika giza nene.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ndipo Sulemani akasema, “Mwenyezi Mungu alisema kwamba ataishi katika giza nene;

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ndipo Sulemani akasema, “bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene;

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ndipo Sulemani akanena, BWANA alisema ya kwamba atakaa katika giza nene.

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Wafalme 8:12
12 Marejeleo ya Msalaba  

Aliziinamisha mbingu akashuka; Kukawa na giza kuu chini ya miguu yake.


hata makuhani hawakuweza kusimama ili kufanya huduma yao, kwa sababu ya wingu lile; kwa kuwa nyumba ya BWANA ilikuwa imejaa utukufu wa BWANA.


Ezra akakifunua kitabu machoni pa watu wote; (maana alikuwa juu ya watu wote); na hapo alipokifungua, watu wote walisimama;


Mawingu na giza vyamzunguka, Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake.


Basi hao watu wakasimama mbali, naye Musa akalikaribia lile giza kuu Mungu alipokuwapo.


Hakika wewe u Mungu ujifichaye nafsi yako, Ee Mungu wa Israeli, Mwokozi.


BWANA akamwambia Musa, Mwambie Haruni ndugu yako, kwamba asiingie wakati wowote katika mahali patakatifu ndani ya pazia, mbele ya kiti cha rehema, kilicho juu ya sanduku, asije akafa; maana, mimi nitaonekana katika lile wingu juu ya kiti cha rehema.


Mkakaribia, mkasimama chini ya ule mlima; mlima ukawaka moto mpaka kati ya mbinguni, kwa giza na mawingu, na giza kuu.


Haya ndiyo maneno ambayo BWANA aliwaambia mkutano wenu wote mlimani kwa sauti kuu toka kati ya moto, na wingu, na giza kuu; wala hakuongeza neno. Akayaandika juu ya mbao mbili za mawe, akanipa.


Maana hamkufikia mlima uwezao kuguswa, uliowaka moto, wala wingu jeusi, na giza, na tufani,