Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 83:4 - Swahili Revised Union Version

4 Wamesema, Njoni, tuwakatilie mbali wasiwe taifa, Na jina la Israeli halitakumbukwa tena.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 Wanasema: “Njoni tuliangamize taifa lao, jina la Israeli lisikumbukwe tena.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 Wanasema: “Njoni tuliangamize taifa lao, jina la Israeli lisikumbukwe tena.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 Wanasema: “Njoni tuliangamize taifa lao, jina la Israeli lisikumbukwe tena.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 Wanasema, “Njooni, tuwaangamize kama taifa, ili jina la Israeli lisikumbukwe tena.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 Wanasema, “Njooni, tuwaangamize kama taifa, ili jina la Israeli lisikumbukwe tena.”

Tazama sura Nakili




Zaburi 83:4
14 Marejeleo ya Msalaba  

Akanena mbele ya nduguze na mbele ya jeshi la Samaria, akisema, Wayahudi hawa wanyonge wanafanyaje? Je! Watajitengenezea boma? Watatoa dhabihu? Au watamaliza katika siku moja? Je! Watayafufua mawe katika chungu hizi za kifusi, nayo yameteketezwa kwa moto?


Walisema mioyoni mwao, Na tuwaangamize kabisa; Mahali penye mikutano ya Mungu Wamepachoma moto katika nchi pia.


Haya! Na tuwatendee kwa akili, wasije wakaongezeka; tena, ikitokea vita, wao nao wasije wakashikamana na adui zetu na kupigana nasi, na kutoka katika nchi hii.


Tuwameze hai kama kuzimu, Na wazima, kama wao washukao shimoni.


Lakini mimi nilikuwa kama mwana-kondoo mpole, achukuliwaye kwenda kuchinjwa; wala sikujua ya kuwa wamefanya mashauri kinyume changu, wakisema, Na tuuharibu mti pamoja na matunda yake, na tumkatilie mbali atoke katika nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.


Amri hizi zikiondoka, zisiwe mbele zangu, asema BWANA, ndipo wazao wa Israeli nao wataacha kuwa taifa mbele zangu milele.


Sifa za Moabu haziko tena; katika Heshboni wameazimia mabaya juu yake, Haya! Njooni, na tumkatilie mbali asiwe taifa. Wewe nawe, Ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.


Bwana MUNGU asema hivi; Itakuwa katika siku hiyo, mawazo yataingia moyoni mwako, nawe utakusudia kusudi baya;


Naye atanena maneno kinyume chake Aliye Juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye Juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa nyakati tatu na nusu


Lakini ili neno hili lisije likaenea katika watu, na tuwatishe wasiseme tena na mtu yeyote kwa jina hili.


ndipo walipojikutanisha pamoja wenyewe kwa wenyewe, ili kupigana na Yoshua, na hao Israeli, kwa nia moja.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo