Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 7:16 - Swahili Revised Union Version

16 Madhara yake yatamrejea kichwani pake, Na dhuluma yake itamshukia utosini.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

16 Uharibifu wake utamrudia yeye mwenyewe; ukatili wake utamwangukia yeye binafsi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

16 Uharibifu wake utamrudia yeye mwenyewe; ukatili wake utamwangukia yeye binafsi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

16 Uharibifu wake utamrudia yeye mwenyewe; ukatili wake utamwangukia yeye binafsi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

16 Ghasia anazozianzisha humrudia mwenyewe, ukatili wake humrudia kichwani.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

16 Ghasia azianzishazo humrudia mwenyewe, ukatili wake humrudia kichwani.

Tazama sura Nakili




Zaburi 7:16
21 Marejeleo ya Msalaba  

Naye BWANA atamrudishia damu yake kichwani pake mwenyewe, kwa kuwa aliwapiga watu wawili wenye haki, na wema kuliko yeye, akawaua kwa upanga, wala babangu Daudi hakujua habari hiyo; yaani Abneri, mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Israeli, na Amasa, mwana wa Yetheri, jemadari wa jeshi la Yuda.


Ukamwambie, ukisema, BWANA asema hivi, Je! Umeua, ukatamalaki? Nawe utamwambia, kusema, BWANA asema hivi, Mahali pale mbwa walipoiramba damu ya Nabothi, mbwa watairamba na damu yako, naam, damu yako.


Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia.


bali mfalme alipoarifiwa, aliamuru kwa barua ya kwamba huo mpango mwovu alioufanya juu ya Wayahudi umrudie kichwani pake mwenyewe; na ya kwamba yeye na wanawe watundikwe juu ya mti.


Kama mimi nilivyoona, hao walimao maovu, Na kupanda madhara, huvuna yayo hayo.


Wabaya na waanguke katika nyavu zao wenyewe, Wakati ninapopita salama.


Uharibifu na umpate kwa ghafla, Na wavu aliouficha umnase yeye mwenyewe; Kwa uharibifu aanguke ndani yake.


Huko ndiko walikoanguka wafanyao maovu; Wameangushwa chini wasiweze kusimama.


Huwaza maovu kitandani pake, Hujiweka katika njia mbaya; hauchukii ubaya.


Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti, Moyo wangu ni thabiti. Nitaimba, nitaimba kwa sauti nzuri,


BWANA amejidhihirisha na kutekeleza hukumu; Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake.


Ndivyo zilivyo njia za kila mwenye tamaa ya mali; Huuondoa uhai wao walio nayo.


Achimbaye shimo atatumbukia mwenyewe; Naye abingirishaye jiwe litamrudia.


Mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake; Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.


Naye Daudi alifahamu ya kuwa Sauli amemkusudia mabaya; akamwambia Abiathari, kuhani, Lete hapa hiyo naivera.


Daudi akasema, Aishivyo BWANA, BWANA atampiga; au siku yake ya kufa itampata; atashuka kwenda vitani na kupotea.


Tena pamoja na wewe BWANA atawatia Israeli mikononi mwa Wafilisti; hata na kesho wewe na wanao mtakuwapo pamoja nami; tena BWANA atawatia jeshi la Israeli pia mikononi mwa Wafilisti.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo