Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yohana 5:40 - Swahili Revised Union Version

40 Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

40 Hata hivyo, nyinyi hamtaki kuja kwangu ili mpate uhai.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

40 Hata hivyo, nyinyi hamtaki kuja kwangu ili mpate uhai.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

40 Hata hivyo, nyinyi hamtaki kuja kwangu ili mpate uhai.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

40 Lakini mnakataa kuja kwangu ili mpate uzima.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

40 Lakini mnakataa kuja kwangu ili mpate uzima.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

40 Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima.

Tazama sura Nakili




Yohana 5:40
23 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu, Wala Israeli hawakunitaka.


BWANA, mkombozi wa Israeli, Mtakatifu wake, amwambia hivi yeye anayedharauliwa na wanadamu; yeye anayechukiwa na taifa hili; yeye aliye mtumishi wao watawalao; Wafalme wataona, watasimama; wakuu nao watasujudu; kwa sababu ya BWANA aliye mwaminifu, Mtakatifu wa Israeli aliyekuchagua.


Basi, nilipokuja, mbona hapakuwa na mtu? Nilipoita, mbona hapakuwa na mtu aliyenijibu? Je! Mkono wangu ni mfupi, hata nisiweze kukomboa? Au je! Mimi sina nguvu za kuponya? Tazama, kwa kukemea kwangu naikausha bahari, mito ya maji naifanya kuwa jangwa; samaki wao wanuka kwa sababu hapana maji, nao wafa kwa kiu.


Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.


Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku awakusanyavyo pamoja vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!


Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.


Mwizi huja tu kuiba, kuua na kuharibu; mimi nilikuja ili wawe na uzima, tena wawe nao tele.


Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.


Mnayachunguza maandiko kwa sababu mnadhani kuwa ndani yake ninyi mna uzima wa milele; na maandiko yayo hayo ndiyo yanayonishuhudia.


Mimi siupokei utukufu kwa wanadamu.


Mnawezaje kuamini ninyi mnaopokeana utukufu ninyi kwa ninyi, na utukufu ule utokao kwa Mungu aliye wa pekee hamwutafuti?


Msikitendee kazi chakula chenye kuharibika, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele; ambacho Mwana wa Adamu atawapa, kwa sababu huyo ndiye aliyetiwa mhuri na Baba, yaani, Mungu.


Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala yeyote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe.


Kwa kuwa mapenzi yake Baba yangu ni haya, ya kwamba kila amtazamaye Mwana na kumwamini yeye, awe na uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.


Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.


Roho na Bibi arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo