Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yohana 5:22 - Swahili Revised Union Version

22 Tena Baba hamhukumu mtu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

22 Baba hamhukumu mtu yeyote; shughuli yote ya hukumu amemkabidhi Mwana,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

22 Baba hamhukumu mtu yeyote; shughuli yote ya hukumu amemkabidhi Mwana,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

22 Baba hamhukumu mtu yeyote; shughuli yote ya hukumu amemkabidhi Mwana,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

22 Wala Baba hamhukumu mtu yeyote, lakini hukumu yote amempa Mwana,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

22 Wala Baba hamhukumu mtu yeyote, lakini hukumu yote amempa Mwana,

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

22 Tena Baba hamhukumu mtu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote;

Tazama sura Nakili




Yohana 5:22
23 Marejeleo ya Msalaba  

Mbele za BWANA, kwa maana anakuja, Kwa maana anakuja aihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, Na mataifa kwa uaminifu wake.


Mbele za BWANA; Kwa maana anakuja kuihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa uaminifu, Na mataifa kwa adili.


Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na kinachotamaniwa na macho yako, lakini ujue wewe ya kwamba kwa ajili ya hayo yote Mungu atakuleta hukumuni.


Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.


Akasema, Nimekabidhiwa vyote na Baba yangu; wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana, na yeyote ambaye Mwana apenda kumfunulia.


Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.


Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.


kama vile ulivyompa mamlaka juu ya watu wote, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele.


Baba ampenda Mwana, naye amempa vyote mkononi mwake.


Naye akampa amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu.


Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu.


Akatuagiza tuwahubirie watu na kushuhudia ya kuwa huyu ndiye aliyeamriwa na Mungu awe Mhukumu wa walio hai na wafu.


Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa mambo haya kwa kumfufua katika wafu.


katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na Injili yangu, kwa Kristo Yesu.


Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee malipo ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyotenda, yawe ni mema au mabaya.


Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake;


Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo