Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yohana 13:34 - Swahili Revised Union Version

34 Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

34 Nawapeni amri mpya: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

34 Nawapeni amri mpya: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

34 Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

34 “Amri mpya nawapa: Mpendane. Kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

34 “Amri mpya nawapa: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

34 Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.

Tazama sura Nakili




Yohana 13:34
38 Marejeleo ya Msalaba  

Mimi ni mwenzi wa watu wote wakuchao, Na wale wayatiio mausia yako.


Nao watakatifu waliopo duniani, ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.


Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi BWANA.


Mgeni aishiye pamoja nawe atakuwa kama mzaliwa kwenu; mpende kama nafsi yako; kwa maana ninyi mlikuwa wageni katika nchi ya Misri; Mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.


lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,


Haya nawaamuru ninyi, mpate kupendana.


Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu;


Pendo halimfanyii jirani neno baya; basi pendo ndilo utimilifu wa sheria.


Msiwiwe na mtu chochote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria.


Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,


Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutotahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.


Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.


Mchukuliane mizigo na hivyo kuitimiza sheria ya Kristo.


mkaende katika upendo, kama Kristo naye alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato.


tangu tuliposikia habari za imani yenu katika Kristo Yesu, na upendo mlio nao kwa watakatifu wote;


Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;


Ndugu, imetupasa kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, kama ilivyo wajibu, kwa kuwa imani yenu inazidi sana, na upendo wa kila mtu kwenu kwa mwenzake umekuwa mwingi.


Upendano wa ndugu na udumu.


Lakini mkiitimiza ile sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa, Mpende jirani yako kama nafsi yako, mwatenda vema.


Mkiisha kujitakasa roho zenu kwa kuitii kweli, hata kuufikia upendano wa ndugu usio na unafiki, basi jitahidini kupendana kwa moyo safi.


na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, upendo.


Maana, hii ndiyo habari mliyoisikia tangu mwanzo, kwamba tupendane sisi kwa sisi;


Na hii ndiyo amri yake, kwamba tuliamini jina la Mwana wake Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi, kama alivyotupa amri.


Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.


Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo