Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yohana 12:10 - Swahili Revised Union Version

10 Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri la kumwua Lazaro naye;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Makuhani wakuu waliamua pia kumwua Lazaro,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Makuhani wakuu waliamua pia kumwua Lazaro,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Makuhani wakuu waliamua pia kumwua Lazaro,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Kwa hiyo viongozi wa makuhani wakapanga njama ya kumuua Lazaro pia,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Kwa hiyo viongozi wa makuhani wakafanya mpango wa kumuua Lazaro pia,

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

10 Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri la kumwua Lazaro naye;

Tazama sura Nakili




Yohana 12:10
14 Marejeleo ya Msalaba  

Basi Musa na Haruni wakaingia kwa Farao, na kumwambia, BWANA, Mungu wa Waebrania, asema hivi, Je! Utakataa hata lini kujinyenyekeza mbele zangu? Wape watu wangu ruhusa waende zao, ili wanitumikie.


Baa hilo ni katika mambo yote yanayofanyika chini ya jua, ya kuwa wote wanalo tukio moja; naam, zaidi ya hayo, mioyo ya wanadamu imejaa maovu, na wazimu umo mioyoni mwao wakati walipo hai, na baadaye huenda kwa wafu.


Lakini wale Mafarisayo wakatoka wakafanya shauri juu yake jinsi ya kumwangamiza.


Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale majusi, alighadhibika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wa kiume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake kote, kuanzia wenye miaka miwili na chini yake, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale majusi.


Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishika hata mtu akifufuka katika wafu.


Na wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri ya kwamba mtu akimjua alipo, alete habari, ili wapate kumkamata.


maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walijitenga, wakamwamini Yesu.


Basi watu wengi katika Wayahudi walipata kujua ya kuwa yeye yuko huko, nao wakaja, si kwa ajili yake Yesu tu, ila wamwone na Lazaro, ambaye Yesu alimfufua katika wafu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo