Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yohana 10:2 - Swahili Revised Union Version

2 Aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 Lakini anayeingia kwa kupitia mlangoni, huyo ndiye mchungaji wa kondoo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 Lakini anayeingia kwa kupitia mlangoni, huyo ndiye mchungaji wa kondoo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 Lakini anayeingia kwa kupitia mlangoni, huyo ndiye mchungaji wa kondoo.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 Yeye anayeingia kupitia kwenye lango ndiye mchungaji wa kondoo.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 Yeye anayeingia kwa kupitia kwenye lango ndiye mchungaji wa kondoo.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

2 Aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo.

Tazama sura Nakili




Yohana 10:2
25 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.


Wewe uchungaye Israeli, usikie, Wewe umwongozaye Yusufu kama kundi; Wewe uketiye juu ya makerubi, utoe nuru.


Maneno yao wenye hekima huwa mfano wa michokoo; na kama misumari iliyogongomewa sana; ndivyo yalivyo maneno yao walio wakuu wa makusanyiko, ambayo yatoka kwa mchungaji mmoja.


Atalilisha kundi lake kama mchungaji, Atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake; Na kuwachukua kifuani mwake, Nao wanyonyeshao atawaongoza polepole.


Ndipo alipozikumbuka siku za kale, za Musa, na watu wake, akisema, Yuko wapi yeye aliyewapandisha toka baharini pamoja na wachungaji wa kundi lake? Yuko wapi yeye aliyetia kati yao Roho yake Mtakatifu?


Nami nitaweka mchungaji mmoja juu yao, naye atawalisha, naam, mtumishi wangu, Daudi; yeye atawalisha, naye atakuwa mchungaji wao.


Na mtu huyu atakuwa amani yetu; wakati Mwashuri atakapoingia katika nchi yetu, na kuyakanyaga majumba yetu, hapo mtawaleta wachungaji saba juu yake, na wakuu wanane.


Sikiza, maombolezo ya wachungaji, Kwa maana utukufu wao umeharibiwa; Sikiza, ngurumo za simba, Kwa maana vichaka vya Yordani vimeharibiwa!


ambalo wenye kundi hilo huwachinja, kisha hujiona kuwa hawana hatia; na hao wawauzao husema, Na ahimidiwe BWANA, kwa maana mimi ni tajiri; na wachungaji wao wenyewe hawawahurumii.


Nami nikawakatilia mbali wachungaji watatu katika mwezi mmoja; maana nafsi yangu ilikuwa imechoka kwa ajili yao, na nafsi zao pia walinichukia.


Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu, na juu ya mtu aliye mwenzangu, asema BWANA wa majeshi; mpige mchungaji, nao kondoo watatawanyika; nami nitaugeuza mkono wangu juu ya wadogo.


Sikilizeni, mfahamu; Sicho kiingiacho kinywani kimtiacho mtu unajisi; bali kitokacho kinywani ndicho kimtiacho mtu unajisi.


Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi;


Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo.


Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.


Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.


Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono na wazee.


Kwa sababu hii nilikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuwateua wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru;


Basi, Mungu wa amani aliyemleta tena kutoka kwa wafu Mchungaji Mkuu wa kondoo, kwa damu ya agano la milele, yeye Bwana wetu Yesu,


Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu.


Na Mchungaji mkuu atakapodhihirishwa, mtalipokea taji la utukufu, lile lisilokauka.


Siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia, na ya vile vinara saba vya dhahabu. Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba; na vile vinara saba ni makanisa saba.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo