Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yoeli 2:18 - Swahili Revised Union Version

18 Hapo ndipo BWANA alipoona wivu kwa ajili ya nchi yake, akawahurumia watu wake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

18 Ndipo Mwenyezi-Mungu akaipenda nchi yake akawahurumia watu wake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

18 Ndipo Mwenyezi-Mungu akaipenda nchi yake akawahurumia watu wake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

18 Ndipo Mwenyezi-Mungu akaipenda nchi yake akawahurumia watu wake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

18 Kisha Mwenyezi Mungu atakuwa na wivu kwa ajili ya nchi yake na kuwa na huruma juu ya watu wake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

18 Kisha bwana atakuwa na wivu kwa ajili ya nchi yake na kuwa na huruma juu ya watu wake.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

18 Hapo ndipo BWANA alipoona wivu kwa ajili ya nchi yake, akawahurumia watu wake.

Tazama sura Nakili




Yoeli 2:18
19 Marejeleo ya Msalaba  

Maana mabaki yatatoka katika Yerusalemu, na wao watakaookoka katika mlima wa Sayuni wivu wa BWANA utatimiza jambo hilo.


Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo BWANA anavyowahurumia wamchao.


Bali fadhili za BWANA ni kwa wamchao Tangu milele hata milele, Na haki yake ni kwa vizazi vyote;


Maana katika Yerusalemu yatatoka mabaki, nao watakaookoka katika mlima Sayuni; wivu wa BWANA wa majeshi utatimiza mambo hayo.


BWANA atatokea kama shujaa; Ataamsha wivu kama mtu wa vita; Atalia, naam, atapiga kelele; Atawatenda adui zake mambo makuu.


Na wageni watajenga kuta zako, Na wafalme wao watakuhudumu; Maana katika ghadhabu yangu nilikupiga, Lakini katika upendeleo wangu nimekurehemu.


Tazama toka mbinguni, ukaone toka makao ya utukufu wako na fahari yako; uko wapi wivu wako, na uweza wako? Shauku ya moyo wako, na huruma zako zimezuiliwa kwangu.


Katika mateso yao yote yeye aliteswa, na malaika wa uso wake akawaokoa; kwa mapenzi yake, na huruma zake, aliwakomboa mwenyewe; akawainua, akawachukua siku zote za kale.


Je! Efraimu siye mwanangu mpendwa? Je! Siye mtoto apendezaye? Maana kila nisemapo neno juu yake, ningali nikimkumbuka sana; kwa sababu hiyo moyo wangu unataabika kwa ajili yake; bila shaka nitamrehemu, asema BWANA.


Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.


Basi yule malaika aliyesema nami akaniambia, Haya, piga kelele na kusema, BWANA wa majeshi asema hivi, Naona wivu kwa ajili ya Yerusalemu, na kwa ajili ya Sayuni; naona wivu mkuu sana.


BWANA wa majeshi asema hivi, Mimi nina wivu kwa ajili ya Sayuni, wivu mkuu, nami nina wivu kwa ajili yake kwa ghadhabu kuu.


Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa bado mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu.


Wakamtia wivu kwa miungu migeni, Wakamkasirisha kwa machukizo.


Kwa kuwa BWANA atawaamua watu wake, Atawahurumia watumwa wake, Aonapo ya kuwa nguvu zao zimeondoka, Na ya kuwa habaki mtu, aliyefungwa wala asiyefungwa,


Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake; Kwa maana atatwaa kisasi kwa damu ya watumwa wake, Atawatoza kisasi adui zake, Tena atafanya kafara kwa nchi yake, na watu wake.


Angalieni, twawaita heri wao waliostahimili. Mmesikia habari za kustahimili kwake Ayubu, kuona mwisho Bwana aliyomtendea, jinsi Bwana alivyo mwingi wa rehema na mwenye huruma.


Nao wakaiondoa hiyo miungu ya kigeni iliyokuwa kati yao, nao wakamtumikia BWANA; na roho yake ilihuzunika kwa sababu ya msiba wa Israeli.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo