Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 7:16 - Swahili Revised Union Version

16 Ninadhoofika; sitaishi sikuzote; Usinisumbue, kwani siku zangu ni uvuvio.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

16 Nayachukia maisha yangu; sitaishi milele. Niacheni, maana siku zangu ni pumzi tu!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

16 Nayachukia maisha yangu; sitaishi milele. Niacheni, maana siku zangu ni pumzi tu!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

16 Nayachukia maisha yangu; sitaishi milele. Niacheni, maana siku zangu ni pumzi tu!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

16 Ninayachukia maisha yangu; nisingetamani kuendelea kuishi. Niache; siku zangu ni ubatili.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

16 Ninayachukia maisha yangu; nisingetamani kuendelea kuishi. Niache; siku zangu ni ubatili.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

16 Ninadhoofika; sitaishi siku zote; Usinisumbue, kwani siku zangu ni uvuvio.

Tazama sura Nakili




Yobu 7:16
22 Marejeleo ya Msalaba  

Rebeka akamwambia Isaka, Rohoni mwangu sina raha kwa sababu ya hao binti za Hethi. Kama Yakobo akitwaa mke katika binti za Hethi, kama hawa binti za nchi, maisha yangu yatanifaidi nini?


Lakini yeye mwenyewe akaendelea katika jangwa mwendo wa siku moja, akaenda akaketi chini ya mretemu. Akajiombea roho yake afe, akasema, Yatosha; sasa, Ee BWANA, uiondoe roho yangu; kwa kuwa mimi si mwema kuliko baba zangu.


Nayachukia maisha yangu; Nitayasema malalamiko yangu wazi; Nitanena kwa uchungu wa roho yangu.


Je! Siku zangu si chache? Acha basi, Usinisumbue, nipate angaa kutulizwa moyo kidogo.


Acha kumwangalia yeye, apate kupumzika, Hata atakapoitimiza siku yake, kama aliyeajiriwa.


Kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda; Kwamba angeulegeza mkono wake na kunikatilia mbali!


Hata nafsi yangu huchagua kunyongwa, Na kuchagua kifo kuliko maumivu yangu haya.


Kumbuka ya kwamba maisha yangu ni upepo; Jicho langu halitaona mema tena.


Mimi ni mkamilifu; siangalii nafsi yangu; Naudharau uhai wangu.


Binadamu ni kama ubatili, Siku zake ni kama kivuli kipitacho.


Uniondolee pigo lako; Kwa mapigo ya mkono wako nimeangamia.


Uache kunitazama, ndio nipate kufurahi tena, Kabla sijafa na kutoweka kabisa.


Kweli, watu wote hupita kama kivuli; Wao hujisumbua bure tu; Wanajirundikia mali wala hawajui ni nani atakayeirithi.


Hakika binadamu ni ubatili, Na wenye cheo ni uongo, Katika mizani huinuka; Wote pamoja ni hafifu kuliko ubatili.


Kwa hiyo akazikomesha siku zao kama pumzi, Na miaka yao kwa hofu ya kuwastusha.


Akakumbuka ya kuwa wao ni kiwiliwili, Upepo upitao wala haurudi.


Basi, nikauchukia uhai; kwa sababu kazi inayotendeka chini ya jua ilikuwa mbaya kwangu; yaani, mambo yote ni ubatili na kufukuza upepo.


Na kufa kutachaguliwa kuliko kuishi na mabaki wote waliosalia katika jamaa hii mbovu, waliosalia kila mahali nilikowafukuza, asema BWANA wa majeshi.


Basi, sasa, Ee BWANA, nakuomba, uniondolee uhai wangu; maana ni afadhali nife mimi kuliko kuishi.


Basi ikawa, jua lilipopanda juu, Mungu akatayarisha upepo wa mashariki, wenye joto jingi; jua likampiga Yona kichwani, hata akazimia, naye akajitakia kufa, akasema, Ni afadhali nife mimi kuliko kuishi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo