Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 10:8 - Swahili Revised Union Version

8 Lakini wote pia huwa kama wanyama, ni wapumbavu. Haya ni maelezo ya sanamu, ni shina la mti tu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Wote ni wajinga na wapumbavu mafunzo ya vinyago ni upuuzi mtupu!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Wote ni wajinga na wapumbavu mafunzo ya vinyago ni upuuzi mtupu!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Wote ni wajinga na wapumbavu mafunzo ya vinyago ni upuuzi mtupu!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Wote hawana akili, tena ni wapumbavu; wanafundishwa na sanamu batili za miti.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Wote hawana akili, tena ni wapumbavu, wanafundishwa na sanamu za miti zisizofaa lolote.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

8 Lakini wote pia huwa kama wanyama, ni wapumbavu. Haya ni maelezo ya sanamu, ni shina la mti tu.

Tazama sura Nakili




Yeremia 10:8
16 Marejeleo ya Msalaba  

Wazitengenezao watafanana nazo, Sawa na wote wanaozitumainia.


Wazifanyao watafanana nazo, Na kila mmoja anayezitumainia.


Tazama, hao wote ni ubatili; kazi zao si kitu; sanamu zao ni upepo mtupu.


Hawajui wala hawafikiri; maana amewafumba macho, wasione, na mioyo yao, wasiweze kufahamu.


Wala hapana atiaye moyoni, wala hapana maarifa, wala fahamu kusema, Nimeteketeza sehemu motoni, naam, pia nimeoka mkate juu ya makaa yake; nimeoka nyama nikaila; nami, je! Kilichobaki nikifanye kuwa chukizo? Je! Nisujudie shina la mti?


Kila mtu amekuwa kama mnyama, hana maarifa; Kila mfua dhahabu amefedheheshwa na sanamu yake ya kuchonga; Maana sanamu yake ya kuyeyuka ni uongo, Wala hamna pumzi ndani yake.


waliambiao gogo la mti, Wewe u baba yangu; na kuliambia jiwe, Ndiwe uliyenizaa; kwa maana wamenipa mimi visogo, wala hawakunielekezea nyuso zao; lakini wakati wa taabu watasema, Simama ukatuokoe.


Hata ikawa, kwa sababu alikuwa mwepesi wa kufanya ukahaba, nchi ikatiwa unajisi, naye akazini na mawe na miti.


Kwa maana watu wangu ni wapumbavu, hawanijui; ni watoto waliopungukiwa na akili, wala hawana ufahamu; ni wenye akili katika kutenda mabaya, bali katika kutenda mema hawana maarifa.


Ndipo nikasema, Hakika, hawa ni maskini; ni wajinga hawa; maana hawaijui njia ya BWANA, wala hukumu ya Mungu wao;


Watu wangu hutaka shauri kwa kipande cha mti, na fimbo yao huwatolea uaguzi; maana roho ya uzinzi imewapotosha, wakawacha Mungu wao.


Watu waangaliao mambo ya ubatili na uongo Hujitenga na rehema zao wenyewe.


Sanamu ya kuchonga yafaa nini, baada ya aliyeifanya ameichonga? Sanamu ya kuyeyuka, nayo ni mwalimu wa uongo, yafaa nini, hata yeye aliyeifanya aiwekee tumaini lake, na kufanya sanamu zisizoweza kusema?


Kwa maana vinyago vimenena maneno ya ubatili, nao waaguzi wameona uongo; nao wameleta habari za ndoto za uongo, wafariji bure; kwa sababu hiyo watu wanatangatanga kama kondoo, wanateseka kwa kukosa mchungaji.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo