Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yakobo 1:11 - Swahili Revised Union Version

11 Maana jua huchomoza kwa joto kali, huyakausha majani; ua lake huanguka, uzuri wa umbo lake hupotea; vivyo hivyo naye tajiri atanyauka katika njia zake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

11 Jua huchomoza na kwa joto lake kali hukausha mimea, nayo maua yake huanguka, na uzuri wake wote huharibika. Vivyo hivyo, tajiri ataangamizwa katika shughuli zake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

11 Jua huchomoza na kwa joto lake kali hukausha mimea, nayo maua yake huanguka, na uzuri wake wote huharibika. Vivyo hivyo, tajiri ataangamizwa katika shughuli zake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

11 Jua huchomoza na kwa joto lake kali hukausha mimea, nayo maua yake huanguka, na uzuri wake wote huharibika. Vivyo hivyo, tajiri ataangamizwa katika shughuli zake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

11 Kwa maana jua kali huchomoza na kuyakausha majani ya mmea, nalo ua lake linaanguka, na uzuri wake unaharibika. Vivyo hivyo tajiri naye atanyauka akiwa anaendelea na shughuli zake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

11 Kwa maana jua kali lenye kuchoma huchomoza na kuliunguza, likayakausha majani, na ua lake likapukutika, nao uzuri wake huharibika. Vivyo hivyo tajiri naye atanyauka akiwa anaendelea na shughuli zake.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

11 Maana jua huchomoza kwa joto kali, huyakausha majani; ua lake huanguka, uzuri wa umbo lake hupotea; vivyo hivyo naye tajiri atanyauka katika njia zake.

Tazama sura Nakili




Yakobo 1:11
27 Marejeleo ya Msalaba  

Wageni nao waliishiwa nguvu, Wakatoka katika ngome zao wakitetemeka.


Siku zangu ni kama kivuli cha jioni, Nami ninanyauka kama majani.


Moyo wangu umepigwa kama majani na kukauka, Naam, ninasahau kula chakula changu.


Mwanadamu siku zake zi kama majani; Kama ua la kondeni ndivyo anavyostawi.


Maana kama majani watakatika mara, Kama miche mibichi watanyauka.


Kweli, watu wote hupita kama kivuli; Wao hujisumbua bure tu; Wanajirundikia mali wala hawajui ni nani atakayeirithi.


Asubuhi yachipuka na kumea, Jioni yakatika na kukauka.


Alivyotoka tumboni mwa mamaye, atakwenda tena tuputupu kama alivyokuja; asichume kitu chochote kwa ajili ya kazi yake, hata akichukue mkononi mwake.


Ole wa taji la kiburi la walevi wa Efraimu, na ua la uzuri wa fahari yake linalonyauka, lililo kichwani mwa bonde linalositawi, la hao walioshindwa na divai!


na ua la uzuri wa fahari yake linalonyauka, lililo kichwani mwa bonde linalositawi, litakuwa kama tini iliyotangulia kuiva kabla ya wakati wa joto, ambayo, aionapo yeye aiangaliaye, huila mara anapoishika mkononi mwake.


Hawataona njaa, wala hawataona kiu; joto halitawapiga, wala jua; kwa maana yeye aliyewarehemu atawatangulia, naam, karibu na chemchemi za maji atawaongoza.


Lakini jua lilipozuka ziliungua; na kwa kuwa hazina mizizi zikanyauka.


wakisema, Hao wa mwisho wamefanya kazi saa moja tu, nawe umewasawazisha na sisi tuliostahimili taabu na joto la mchana kutwa.


Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa katika tanuri, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?


hata jua lilipozuka iliungua, na kwa kuwa haina mizizi ikanyauka.


Na wale wautumiao ulimwengu huu, kama hawautumii sana; kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita.


tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu.


Na Mchungaji mkuu atakapodhihirishwa, mtalipokea taji la utukufu, lile lisilokauka.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo