Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Walawi 26:11 - Swahili Revised Union Version

11 Nami nitaiweka maskani yangu kati yenu; wala roho yangu haitawachukia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

11 Nitaweka maskani yangu miongoni mwenu, wala sitawaacheni.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

11 Nitaweka maskani yangu miongoni mwenu, wala sitawaacheni.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

11 Nitaweka maskani yangu miongoni mwenu, wala sitawaacheni.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

11 Nitafanya makao yangu miongoni mwenu, nami sitawachukia.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

11 Nitafanya makao yangu miongoni mwenu, nami sitawachukia.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

11 Nami nitaiweka maskani yangu kati yenu; wala roho yangu haitawachukia.

Tazama sura Nakili




Walawi 26:11
27 Marejeleo ya Msalaba  

Mahali kote nilikokwenda na wana wa Israeli wote, je! Nimesema neno lolote na mtu yeyote wa waamuzi wa Israeli, niliyemwagiza kuwalisha watu wangu Israeli, nikisema, Mbona hamkunijengea nyumba ya mierezi?


Nami nitakaa katikati ya wana wa Israeli, wala sitawaacha watu wangu Israeli.


Hakika nimekujengea nyumba ya kukaa, iwe mahali pa makao yako milele.


Lakini Mungu je? Hakika atakaa juu ya nchi? Tazama, mbingu hazikutoshi, wala mbingu za mbingu; sembuse nyumba hii niliyoijenga!


Hasira ya BWANA ikawaka juu ya watu wake, Akauchukia urithi wake.


Kibanda chake pia kiko Salemu, Na maskani yake iko Sayuni.


Mungu alisikia, akaghadhibika, Akamkataa Israeli kabisa.


Nao na wanifanyie patakatifu; ili nipate kukaa kati yao.


Na mimi nitakaa kati ya wana wa Israeli, nami nitakuwa Mungu wao.


Nao watanijua kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wao, niliyewatoa katika nchi ya Misri, nipate kukaa kati yao; ni mimi BWANA Mungu wao.


Usituchukie, kwa ajili ya jina lako; usikifedheheshe kiti cha enzi cha utukufu wako, kumbuka, usilivunje agano ulilofanya nasi.


Bwana ameitupilia mbali madhabahu yake, Amepachukia patakatifu pake; Amezitia katika mikono ya hao adui Kuta za majumba yake; Wamepiga kelele ndani ya nyumba ya BWANA Kama katika sikukuu.


Nanyi mtajua ya kuwa mimi ni katikati ya Israeli, na ya kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu, wala hakuna mwingine; na watu wangu hawatatahayari kamwe.


Nanyi msiende kwa kuzifuata desturi za taifa, niitoayo mbele yenu; kwa kuwa wao waliyafanya mambo hayo yote, na kwa ajili ya hayo niliwachukia.


nanyi mkizikataa amri zangu, na roho yenu ikichukia amri zangu, hata ikawa hamtaki kuyafanya maagizo yangu yote, bali mwalivunja agano langu;


Nchi nayo itaachwa na wao, nayo itazifurahia Sabato zake, itakapokuwa ukiwa pasipokuwa na wao; nao wataikubali adhabu ya uovu wao; kwa sababu wameyakataa maagizo yangu, na roho zao zimezichukia amri zangu.


Lakini pamoja na hayo yote, watakapokuwa katika nchi ya adui zao, mimi, sitawatupa, wala sitawachukia, niwaangamize kabisa, na kulivunja agano langu pamoja nao; kwa kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wao;


Nami nikawakatilia mbali wachungaji watatu katika mwezi mmoja; maana nafsi yangu ilikuwa imechoka kwa ajili yao, na nafsi zao pia walinichukia.


Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja kuwa maskani ya Mungu katika Roho.


BWANA akaona, akawachukia, Kwa sababu ya kukasirishwa na wanawe na binti zake.


Basi ikiwa hiyo inchi yenu ni najisi, vukeni na kuingia katika nchi ya milki yake BWANA, ambamo maskani ya BWANA inakaa ndani yake, nanyi twaeni milki kati yetu; lakini msimwasi BWANA, wala msituasi sisi, kwa kujijengea madhabahu zaidi ya hiyo madhabahu ya BWANA, Mungu wetu.


Naye Finehasi, mwana wa Eleazari, kuhani, akawaambia wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, na wana wa Manase, akasema, Siku hii ya leo tumejua ya kwamba BWANA yu kati yetu, kwa sababu hamkukosa katika jambo hili mbele ya BWANA; sasa ninyi mmewaokoa wana wa Israeli na mkono wa BWANA.


Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.


Kwa hiyo wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, nao wanamtumikia mchana na usiku katika hekalu lake, na yeye aketiye katika kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo