Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Walawi 10:11 - Swahili Revised Union Version

11 tena mpate kuwafundisha wana wa Israeli amri hizi zote ambazo BWANA amewaambia kwa mkono wa Musa.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

11 Mtawafundisha Waisraeli masharti yote ambayo nimewaambia kwa njia ya Mose.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

11 Mtawafundisha Waisraeli masharti yote ambayo nimewaambia kwa njia ya Mose.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

11 Mtawafundisha Waisraeli masharti yote ambayo nimewaambia kwa njia ya Mose.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

11 na lazima mwafundishe Waisraeli amri zote ambazo Mwenyezi Mungu aliwapa kupitia Musa.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

11 na lazima mwafundishe Waisraeli amri zote ambazo bwana aliwapa kupitia Musa.”

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

11 tena mpate kuwafundisha wana wa Israeli amri hizi zote ambazo BWANA amewaambia kwa mkono wa Musa.

Tazama sura Nakili




Walawi 10:11
16 Marejeleo ya Msalaba  

Basi kwa siku nyingi Israeli wamekuwa hawana Mungu wa kweli, wala hawana kuhani afundishaye, wala hawana torati;


Wakafundisha katika Yuda, wenye kitabu cha Torati ya BWANA; wakazunguka katika miji yote ya Yuda, wakafundisha kati ya watu.


Hezekia akawafurahisha mioyo Walawi wote waliokuwa mastadi wa kumtumikia BWANA. Basi muda wa siku saba wakala sikukuu, wakitoa dhabihu za sadaka za amani, na kumtolea shukrani BWANA, Mungu wa baba zao.


Naye Ezra, kuhani, akaileta Torati mbele ya mkutano mzima, wanaume na wanawake, na wote walioweza kusikia na kufahamu, siku ya kwanza na mwezi wa saba.


Nao wakasoma katika kitabu, katika Torati ya Mungu, kwa sauti ya kusikika; wakaeleza maana yake, hata wakayafahamu yaliyosomwa.


Hapo ndipo waliposema, Njooni na tufanye mashauri juu ya Yeremia; maana sheria haitampotea kuhani, wala shauri halitampotea mwenye hekima, wala neno halitampotea nabii. Njooni, na tumpige kwa ndimi zetu, wala tusiyaangalie maneno yake yoyote.


Makuhani hawakusema, Yuko wapi BWANA? Wala wanasheria hawakunijua; wachungaji nao waliniasi, nao manabii walitoa unabii kwa Baali, wakafuata mambo yasiyofaidia kitu.


Kwa maana yapasa midomo ya kuhani ihifadhi maarifa, tena yawapasa watu kuitafuta sheria kinywani mwake; kwa kuwa yeye ni mjumbe wa BWANA wa majeshi.


na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.


Kwa maana sikujiepusha na kuwahubiria habari ya kusudi lote la Mungu.


nawe fanya sawasawa na hukumu watakayokuonesha mahali hapo atakapochagua BWANA; nawe tunza kufanya kwa mfano wa yote watakayokufunza;


kwa mfano wa sheria watakayokufunza, na kwa mfano wa hukumu watakayokuambia, fanya vivyo hivyo; usigeuke katika hukumu watakayokuonesha, kwenda mkono wa kulia wala wa kushoto.


Angalia katika pigo la ukoma, utunze kwa bidii, kwa kufanya mfano wa yote watakayowafundisha makuhani Walawi; tunzeni kwa kuyafanya vile vile kama nilivyowaamuru wao.


Watamfundisha Yakobo hukumu zako, Na Israeli torati yako, Wataweka uvumba mbele zako, Na sadaka nzima za kuteketezwa madhabahuni mwako.


Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana Yesu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo