Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Wafilipi 3:2 - Swahili Revised Union Version

2 Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na wajikatao.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 Jihadharini na hao watendao maovu, hao mbwa, watu wanaosisitiza kujikata mwilini.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 Jihadharini na hao watendao maovu, hao mbwa, watu wanaosisitiza kujikata mwilini.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 Jihadharini na hao watendao maovu, hao mbwa, watu wanaosisitiza kujikata mwilini.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 Jihadharini na mbwa, wale watenda maovu, jihadharini na wale wajikatao miili yao.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 Jihadharini na mbwa, wale watenda maovu, jihadharini na wale wajikatao miili yao, wasemao ili kuokoka ni lazima kutahiriwa.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

2 Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na wajikatao.

Tazama sura Nakili




Wafilipi 3:2
31 Marejeleo ya Msalaba  

Enyi watenda mabaya, ondokeni kwangu, Niyashike maagizo ya Mungu wangu.


Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenidunga mikono na miguu.


Uniponye nafsi yangu na upanga, Mpenzi wangu na nguvu za mbwa.


Kama vile mbwa arudiavyo matapiko yake; Kadhalika mpumbavu afanya upumbavu tena.


Ndipo wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana, na kuchukiana.


Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya kondoo, lakini kwa ndani ni mbwamwitu wakali.


Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua.


Maana yeye si Myahudi aliye Myahudi kwa nje tu, wala tohara siyo ile ya nje tu katika mwili;


Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo.


Maana ninyi, ndugu, mliitwa mpate uhuru; lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili, bali tumikianeni kwa upendo.


Lakini mkiumana na kulana, angalieni msije mkaangamizana.


Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutotahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.


mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao uko katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.


Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili.


uwe mwenye imani na dhamiri njema, ambayo wengine wameisukumia mbali, wakaangamia katika Imani.


Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala hawafai kwa tendo lolote jema.


Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaagaa matopeni.


Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.


Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani.


Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.


Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.


Tazama, nakupa walio wa sinagogi la Shetani, wasemao kwamba ni Wayahudi, nao sio, bali wasema uongo. Tazama, nitawafanya waje kusujudu mbele ya miguu yako, na kujua ya kuwa nimekupenda.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo