Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Wafilipi 3:11 - Swahili Revised Union Version

11 ili nipate kwa njia yoyote kuufikia ufufuo wa wafu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

11 nikitumaini kwamba nami pia nitafufuliwa kutoka kwa wafu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

11 nikitumaini kwamba nami pia nitafufuliwa kutoka kwa wafu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

11 nikitumaini kwamba nami pia nitafufuliwa kutoka kwa wafu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

11 ili kwa njia yoyote niweze kufikia ufufuo wa wafu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

11 ili kwa njia yoyote niweze kufikia ufufuo wa wafu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

11 ili nipate kwa njia yoyote kuufikia ufufuo wa wafu.

Tazama sura Nakili




Wafilipi 3:11
17 Marejeleo ya Msalaba  

Hakuna mtu awezaye kumkomboa ndugu yake, Wala kumlipa Mungu fidia kwa ajili ya maisha yake,


nawe utakuwa heri, kwa kuwa hao hawana cha kukulipa; kwa maana utalipwa katika ufufuo wa wenye haki.


Martha akamwambia, Najua ya kuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.


Paulo alipotambua ya kuwa sehemu moja ni Masadukayo, na sehemu ya pili ni Mafarisayo, akapaza sauti yake katika ile baraza, Ndugu zangu, mimi ni Farisayo mwana wa Farisayo; mimi ninahukumiwa kwa ajili ya tumaini la ufufuo wa wafu.


ambayo kabila zetu kumi na mbili wanataraji kuifikia, wakimwabudu Mungu kwa bidii mchana na usiku. Nami ninashitakiwa na Wayahudi kwa ajili ya tumaini hilo, Ee Mfalme.


Na kwa sababu bandari ile ilikuwa haifai kukaa wakati wa baridi, wengi wao wakatoa shauri la kutweka kutoka huko ili wapate kufika Foinike, kama ikiwezekana, na kukaa huko wakati wa baridi; nayo ni bandari ya Krete, inaelekea kaskazini mashariki na kusini mashariki.


nipate kuwatia wivu walio damu moja na mimi na kuwaokoa baadhi yao.


Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo; baadaye walio wake Kristo, atakapokuja.


Kwa wanyonge nilikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.


bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiria wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.


Lakini nahofu; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.


Kwa hiyo mimi nami nilipokuwa siwezi kuvumilia tena, nilituma mtu ili niijue imani yenu, asije yule mjaribu akawajaribu, na taabu yetu ikawa haina faida.


Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yoyote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;


baada ya hayo nimewekewa taji la haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.


Wanawake walipokea wafu wao waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora;


Hao wafu waliobakia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo