Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Waefeso 2:1 - Swahili Revised Union Version

1 Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Nyinyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa na dhambi zenu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Nyinyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa na dhambi zenu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Nyinyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa na dhambi zenu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Ninyi mlikuwa wafu katika makosa na dhambi zenu,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Kwa habari zenu, mlikuwa wafu katika makosa na dhambi zenu,

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

1 Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;

Tazama sura Nakili




Waefeso 2:1
21 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA akasikia harufu ya kumridhisha; BWANA akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, maana mawazo ya moyo wa mwanadamu ni mabaya tangu ujana wake; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya. 1


Lakini Yesu akamwambia, Nifuate; waache wafu wazike wafu wao.


kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia.


Bali ilibidi kusherehekea na kushangilia kwa kuwa huyu ndugu yako alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana.


Mwizi huja tu kuiba, kuua na kuharibu; mimi nilikuja ili wawe na uzima, tena wawe nao tele.


Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.


Maana kama Baba awafufuavyo wafu na kuwahuisha, vivyo hivyo na Mwana awahuisha wale awatakao.


Amin, amin, nawaambia, Saa inakuja, na sasa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai.


Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.


Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa kiumbe aliye hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha.


Maana, upendo wa Kristo watuongoza; maana tumehukumu hivi, ya kwamba mmoja alikufa kwa ajili ya wote, basi walikufa wote;


ambao; akili zao zimetiwa giza, nao wametengwa na uzima wa Mungu, kwa sababu ya ujinga uliomo ndani yao, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao;


Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.


Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutotahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;


Bali, yeye asiyejizuia nafsi yake amekufa ingawa yu hai.


Sisi tunajua ya kuwa tumepita toka mautini kuingia uzimani, kwa maana tunawapenda ndugu. Yeye asiyependa, akaa katika mauti.


Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na hizo Roho saba za Mungu, na zile nyota saba. Nayajua matendo yako, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo