Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Waebrania 4:8 - Swahili Revised Union Version

8 Maana kama Yoshua angaliwapa pumziko, asingaliinena siku nyingine baadaye.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Kama Yoshua angekuwa amewapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Kama Yoshua angekuwa amewapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Kama Yoshua angekuwa amewapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Kwa maana kama Yoshua angelikuwa amewapa raha, Mungu hangesema tena baadaye kuhusu siku nyingine.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Kwa maana kama Yoshua alikuwa amewapa raha, Mwenyezi Mungu hangesema tena baadaye kuhusu siku nyingine.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

8 Maana kama Yoshua angaliwapa pumziko, asingaliinena siku nyingine baadaye.

Tazama sura Nakili




Waebrania 4:8
13 Marejeleo ya Msalaba  

na mwanawe huyo ni Nuni, na mwanawe huyo ni Yoshua.


Akawapa nchi za mataifa, wakairithi kazi ya watu;


Akawafukuza mataifa mbele yao, Akawapimia urithi kwa kamba, Na kuwakalisha makabila ya Israeli katika hema zao.


ambayo baba zetu, kwa kupokezana, wakaiingiza pamoja na Yoshua katika milki ya Mataifa wale, ambao Mungu aliwafukuza mbele ya baba zetu, mpaka siku za Daudi;


kwani hamjafikia bado katika raha na urithi akupao BWANA, Mungu wako.


Basi itakuwa, hapo atakapokwisha kukupumzisha BWANA, Mungu wako, katika adui zako wote walio kandokando, katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako, iwe urithi uimiliki, ndipo uufute ukumbuko wa Amaleki chini ya mbingu; usisahau.


Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi,


Basi, limesalia pumziko la sabato kwa watu wa Mungu.


hadi BWANA atakapowapa ndugu zenu raha, kama alivyowapa ninyi, na wao pia wamepata kuimiliki nchi awapayo BWANA, Mungu wenu; ndipo mtakapoirudia nchi ya milki yenu na kuimiliki, ambayo Musa mtumishi wa BWANA aliwapeni ng'ambo ya Yordani upande wa maawio ya jua.


Basi Yoshua akaitwaa hiyo nchi yote, sawasawa na hayo yote BWANA aliyokuwa amemwambia Musa; Yoshua naye akawapa Israeli kuwa ni urithi wao, sawasawa na walivyogawanyikana kwa makabila yao. Kisha nchi ikatulia isiwe na vita tena.


Na sasa yeye BWANA, Mungu wenu, amewapa ndugu zenu kustarehe, kama alivyowaambia; basi sasa rudini ninyi mwende mahemani kwenu, hata nchi ya milki yenu, ambayo huyo Musa, mtumishi wa BWANA, aliwapa ng'ambo ya pili ya Yordani.


Hata ikawa baada ya siku nyingi, BWANA alipokuwa amekwisha kuwapa Israeli amani mbele ya adui zao pande zote, naye Yoshua alipokuwa mzee, mwenye miaka mingi sana,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo