Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Nehemia 9:37 - Swahili Revised Union Version

37 Nayo yawapatia faida nyingi wafalme uliowaweka kututawala kwa sababu ya dhambi zetu; tena wana mamlaka juu ya miili yetu, na juu ya wanyama wetu, kadiri wapendavyo, nasi tuko katika dhiki kuu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

37 Kwa sababu ya dhambi zetu, utajiri wa nchi hii unawaendea wafalme uliowaleta kututawala. Wanatutawala wapendavyo hata na mifugo yetu wanaitendea wapendavyo, tumo katika dhiki kuu.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

37 Kwa sababu ya dhambi zetu, utajiri wa nchi hii unawaendea wafalme uliowaleta kututawala. Wanatutawala wapendavyo hata na mifugo yetu wanaitendea wapendavyo, tumo katika dhiki kuu.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

37 Kwa sababu ya dhambi zetu, utajiri wa nchi hii unawaendea wafalme uliowaleta kututawala. Wanatutawala wapendavyo hata na mifugo yetu wanaitendea wapendavyo, tumo katika dhiki kuu.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

37 Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

37 Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

37 Nayo yawapatia faida nyingi wafalme uliowaweka kututawala kwa sababu ya dhambi zetu; tena wana mamlaka juu ya miili yetu, na juu ya wanyama wetu, kadiri wapendavyo, nasi tuko katika dhiki kuu.

Tazama sura Nakili




Nehemia 9:37
11 Marejeleo ya Msalaba  

Basi, ijulikane kwa mfalme, ya kuwa mji huu ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hawatatoa kodi, wala ada, wala ushuru, na mwisho wake wafalme watapata hasara.


Tena, natoa amri kuwaagiza ninyi mtakayowatendea wazee hao wa Wayahudi, kwa kazi hii ya kuijenga nyumba ya Mungu; kwa mali ya mfalme, yaani, kwa kodi za nchi iliyo ng'ambo ya Mto, watu hao wapewe gharama zote bila kukawia, ili wasizuiliwe.


Tena tunawaarifu ya kuwa katika habari ya makuhani, na Walawi, na waimbaji, na mabawabu na Wanethini, au watumishi wa nyumba hii ya Mungu, si halali kuwatoza kodi, wala ada, wala ushuru.


Nikawaambia, Sisi kwa kadiri ya uwezo wetu tumewakomboa ndugu zetu Wayahudi, waliouzwa kwa makafiri; na ninyi mnataka kuwauza ndugu zenu, tena kuwauza ili sisi tuwanunue? Wakanyamaza kimya, wasiweze kusema neno lolote.


Watufuatiao wako juu ya shingo zetu; Tumechoka, tusipate pumziko lolote.


Nami nitauelekeza uso wangu kinyume chenu, nanyi mtapigwa mbele ya adui zenu; hao wawachukiao watatawala juu yenu; nanyi mtakimbia wakati ambao hapana awafukuzaye.


Wakamjibu, Sisi tu uzao wake Abrahamu, wala hatujawa watumwa wa mtu wakati wowote; nawe wasemaje, Mtawekwa huru?


Matunda ya nchi yako, na taabu yako yote, vitaliwa na taifa usilolijua; utaonewa tu, na kupondwa chini daima;


Utapanda mizabibu na kuitengeza, wala hutakunywa katika divai yake, wala kuichuma kwani italiwa na mabuu.


kwa hiyo utawatumikia adui zako atakaowaleta BWANA juu yako, kwa njaa, na kwa kiu, na kwa uchi, na kwa uhitaji wa vitu vyote; naye atakuvika kongwa la chuma shingoni mwako, hata atakapokwisha kukuangamiza.


naye atakula uzao wa ng'ombe wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako mpaka utakapokwisha kuangamizwa; wala hatakuachia nafaka, wala divai, wala mafuta, wala kuongezeka kwa ng'ombe wako, wala wana-kondoo wako, hata atakapokwisha kukuangamiza.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo