Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Nehemia 9:24 - Swahili Revised Union Version

24 Basi wale watoto wakaingia wakaimiliki nchi, nawe ukawatiisha wenyeji wa nchi mbele yao, ndio Wakanaani, ukawatia mikononi mwao, pamoja na wafalme wao, na watu wa nchi, wawatende kama wapendavyo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

24 Hivyo, hao wazawa wakaja na kuimiliki nchi; uliwashinda wakazi wa nchi hiyo, Wakanaani, ukawatia mikononi mwao, pamoja na wafalme wao, watu wao na nchi yao ili wawatende wapendavyo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

24 Hivyo, hao wazawa wakaja na kuimiliki nchi; uliwashinda wakazi wa nchi hiyo, Wakanaani, ukawatia mikononi mwao, pamoja na wafalme wao, watu wao na nchi yao ili wawatende wapendavyo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

24 Hivyo, hao wazawa wakaja na kuimiliki nchi; uliwashinda wakazi wa nchi hiyo, Wakanaani, ukawatia mikononi mwao, pamoja na wafalme wao, watu wao na nchi yao ili wawatende wapendavyo.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

24 Wana wao wakaingia na kuimiliki nchi. Uliwatiisha Wakanaani mbele yao, walioishi katika nchi, ukawatia Wakanaani mikononi mwao, pamoja na wafalme wao na watu wa nchi, wawafanyie kama wapendavyo.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

24 Wana wao wakaingia na kuimiliki nchi. Uliwatiisha Wakanaani mbele yao, walioishi katika nchi, ukawatia Wakanaani mikononi mwao, pamoja na wafalme wao na watu wa nchi, wawafanyie kama wapendavyo.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

24 Basi wale watoto wakaingia wakaimiliki nchi, nawe ukawatiisha wenyeji wa nchi mbele yao, ndio Wakanaani, ukawatia mikononi mwao, pamoja na wafalme wao, na watu wa nchi, wawatende kama wapendavyo.

Tazama sura Nakili




Nehemia 9:24
13 Marejeleo ya Msalaba  

Je! Si BWANA, Mungu wenu, aliye pamoja nanyi? Na kuwapa amani pande zote? Kwa kuwa wenyeji wa nchi amewatia mkononi mwangu; nayo nchi imetiishwa mbele za BWANA, na mbele ya watu wake.


Basi Wayahudi wakawapiga adui zao wote mapigo ya upanga, na kuwachinja, na kuwaangamiza, wakawatenda kama wapendavyo wale waliowachukia.


Lakini Watoto wenu, ambao mlisema watakuwa mateka, ndio nitakaowaleta na kuwatia ndani, nao wataijua nchi mliyoikataa ninyi.


wapate tena fahamu zao, na kutoka katika mtego wa Ibilisi, ambaye amewanasa, hata wakayafanya mapenzi yake.


Basi Yoshua akaipiga nchi hiyo yote, nchi ya vilima, na nchi ya Negebu, na nchi ya Shefela, na nchi ya materemko, na wafalme wake wote; hakumwacha aliyesalia hata mmoja; lakini akawaharibu kabisa wote waliokuwa hai, kama BWANA, Mungu wa Israeli, alivyoamuru.


Basi Yoshua akaitwaa hiyo nchi yote, sawasawa na hayo yote BWANA aliyokuwa amemwambia Musa; Yoshua naye akawapa Israeli kuwa ni urithi wao, sawasawa na walivyogawanyikana kwa makabila yao. Kisha nchi ikatulia isiwe na vita tena.


mfalme wa Egloni, mmoja; na mfalme wa Gezeri, mmoja;


na mfalme wa Tirza, mmoja; wafalme hao wote walikuwa ni thelathini na mmoja.


Kisha mkutano mzima wa wana wa Israeli walikutana pamoja hapo Shilo, wakasimamisha hema ya kukutania huko; nayo nchi ilikuwa imeshindwa mbele zao.


Basi BWANA aliwapa Israeli nchi hiyo yote, ambayo aliapa kwamba atawapa baba zao; nao wakaimiliki, na kukaa humo.


Halikuanguka neno lolote katika jambo lolote lililokuwa ni jema ambalo BWANA alikuwa amelinena katika habari ya nyumba ya Israeli; yalitimia mambo yote.


Basi hivyo Mungu akamshinda Yabini, mfalme wa Kanaani mbele ya wana wa Israeli siku hiyo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo