Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mwanzo 17:6 - Swahili Revised Union Version

6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 Nitakufanya uwe na wazawa wengi sana; kwako nitazusha mataifa mengi na wafalme.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 Nitakufanya uwe na wazawa wengi sana; kwako nitazusha mataifa mengi na wafalme.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 Nitakufanya uwe na wazawa wengi sana; kwako nitazusha mataifa mengi na wafalme.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana; kwako yatatoka mataifa, na wafalme watatoka kwako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, kwako yatatoka mataifa nao wafalme watatoka kwako.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako.

Tazama sura Nakili




Mwanzo 17:6
15 Marejeleo ya Msalaba  

Na uzao wako nitaufanya uwe kama mavumbi ya nchi; ikiwa mtu ataweza kuyahesabu mavumbi ya nchi, uzao wako nao utahesabika.


Nami nitambariki, na tena nitakupa mwana kwake, naam, nitambariki, naye atakuwa mama wa mataifa, na wafalme wa makabila ya watu watatoka kwake.


Kuhusu Ishmaeli nimekusikia, nimembariki na nitamzidisha na kumwongeza sana. Atakuwa baba wa watawala kumi na wawili, na atakuwa na taifa kuu.


Hili ndilo agano langu nawe, utakuwa baba wa mataifa mengi,


Akaondoka huko akachimba kisima kingine, wala hicho hawakukigombania. Akakiita jina lake Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa BWANA ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi.


Na Mungu Mwenyezi, akubariki, akuzidishe, na kukuongeza, ili uwe mtu wa watu wengi.


Mungu akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uzidi ukaongezeke. Taifa na kundi la mataifa watatoka kwako, na wafalme watatoka katika uzao wako.


Na wa pili akamwita jina lake Efraimu, maana alisema, Mungu amenipa uzazi katika nchi ya mateso yangu.


Israeli akakaa katika nchi ya Misri, katika nchi ya Gosheni. Wakapata mali humo, wakaongezeka na kuzidi sana.


Yakobo akamwambia Yusufu, Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu, katika nchi ya Kanaani, akanibariki,


akaniambia, Mimi hapa, nitakuongezea uzao wako, na kukuzidisha, nami nitakufanya uwe kundi la mataifa; kisha nitawapa wazao wako nchi hii baada yako, iwe milki ya milele.


Tena walikuwako wafalme wakuu juu ya Yerusalemu, waliotawala nchi yote iliyo ng'ambo ya Mto; wakapewa kodi, na ada, na ushuru.


Nami nitawaelekezea uso wangu, na kuwapa uzazi mwingi, na kuwaongeza; nami nitalithibitisha agano langu pamoja nanyi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo