Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mika 3:6 - Swahili Revised Union Version

6 Kwa hiyo itakuwa usiku kwenu, msipate kuona maono; tena itakuwa giza kwenu, msiweze kubashiri; nalo jua litawachwea manabii, nao mchana utakuwa mweusi juu yao.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 “Kwenu manabii kutakuwa usiku bila maono, kutakuwa giza kwenu bila ufunuo. Kwenu manabii kutakuchwa, mchana utakuwa giza kwenu.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 “Kwenu manabii kutakuwa usiku bila maono, kutakuwa giza kwenu bila ufunuo. Kwenu manabii kutakuchwa, mchana utakuwa giza kwenu.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 “Kwenu manabii kutakuwa usiku bila maono, kutakuwa giza kwenu bila ufunuo. Kwenu manabii kutakuchwa, mchana utakuwa giza kwenu.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono, na giza, msiweze kubashiri. Jua litawachwea manabii hao, nao mchana utakuwa giza kwao.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono, na giza, msiweze kubashiri. Jua litawachwea manabii hao, nao mchana utakuwa giza kwao.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

6 Kwa hiyo itakuwa usiku kwenu, msipate kuona maono; tena itakuwa giza kwenu, msiweze kubashiri; nalo jua litawachwea manabii, nao mchana utakuwa mweusi juu yao.

Tazama sura Nakili




Mika 3:6
14 Marejeleo ya Msalaba  

Hatuzioni ishara zetu, wala sasa hakuna nabii, Wala kwetu hakuna ajuaye, hadi lini?


Kwa maana BWANA amewamwagieni roho ya usingizi, amefumba macho yenu, yaani, manabii; amefunika vichwa vyenu, yaani, waonaji.


Twapapasapapasa kutafuta ukuta kama kipofu, naam, twapapasa kama watu wasio na macho; twajikwaa wakati wa adhuhuri, kana kwamba ni wakati wa ukungu wa alfajiri; kati yao walionenepa tumekuwa kama wafu.


Mtukuzeni BWANA, Mungu wenu, kabla hajaleta giza, na kabla miguu yenu haijakwaa juu ya milima yenye giza; na wakati mnapoitazamia nuru, kabla hajaigeuza kuwa kivuli cha mauti, na giza nene.


Mwanamke aliyezaa watoto saba anazimia; ametoa roho; jua lake limekuchwa, ikiwa bado ni wakati wa mchana; ameaibika na kutwezwa; na mabaki yao nitawatoa kwa upanga mbele ya adui zao, asema BWANA.


Hapo ndipo waliposema, Njooni na tufanye mashauri juu ya Yeremia; maana sheria haitampotea kuhani, wala shauri halitampotea mwenye hekima, wala neno halitampotea nabii. Njooni, na tumpige kwa ndimi zetu, wala tusiyaangalie maneno yake yoyote.


Na mkono wangu utakuwa juu ya manabii wanaoona ubatili, na kutabiri uongo; hawatakuwa katika mashauri ya watu wangu, wala hawataandikwa katika maandiko ya nyumba ya Israeli, wala hawataingia katika nchi ya Israeli; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana MUNGU.


Madhara yatakuja juu ya madhara, na habari ya shari juu ya habari ya shari; nao watakwenda kwa nabii kutaka maono; lakini hiyo sheria itampotea kuhani, na mashauri yatawapotea wazee.


Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya BWANA.


Msitabiri, ndivyo watabirivyo; wasiyatabiri mambo haya; lawama hazikomi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo