Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mhubiri 2:22 - Swahili Revised Union Version

22 Kwa maana mtu hupata nini kwa kazi yake yote, na kwa juhudi ya moyo wake alivyojitahidi chini ya jua?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

22 Mtu anafaidi nini kutokana na kazi zake zote, na juhudi anazohangaika nazo duniani?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

22 Mtu anafaidi nini kutokana na kazi zake zote, na juhudi anazohangaika nazo duniani?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

22 Mtu anafaidi nini kutokana na kazi zake zote, na juhudi anazohangaika nazo duniani?

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

22 Mtu atapata nini kwa taabu yote na kuhangaika kwa bidii katika kazi anayotaabikia chini ya jua?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

22 Mtu atapata nini kwa taabu yote na kuhangaika kwa bidii katika kazi anayotaabikia chini ya jua?

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

22 Kwa maana mtu hupata nini kwa kazi yake yote, na kwa juhudi ya moyo wake alivyojitahidi chini ya jua?

Tazama sura Nakili




Mhubiri 2:22
21 Marejeleo ya Msalaba  

Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema, Na kukawia kwenda kulala, Na kula chakula cha taabu; Yeye humpa mpenzi wake usingizi.


Nafsi yake mfanyakazi hujifanyia kazi; Maana kinywa chake humtia bidii.


Mtu ana faida gani ya kazi yake yote aifanyayo chini ya jua?


Kisha nikaziangalia kazi zote zilizofanywa kwa mikono yangu, na taabu yote niliyotaabika katika kuzitenda; na tazama, yote ni ubatili na kufukuza upepo, wala faida hakuna chini ya jua.


Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale anayojishughulisha nayo?


Heri konzi moja pamoja na utulivu, Kuliko konzi mbili pamoja na taabu; na kufukuza upepo.


Kuna mtu aliye peke yake, wala hana mwenzi wake; naam, hana mwana wala ndugu; hata hivyo amali yake haina mwisho, wala macho yake hayashibi utajiri. Basi asema, Ni kwa ajili ya nani nafanya kazi, na kujinyima nafsi yangu mema? Hayo nayo ni ubatili, naam, ni taabu kubwa.


Siku zake zote hula gizani, mwenye fadhaa nyingi, mwenye ugonjwa na uchungu.


Kisha nikaisifu furaha, kwa sababu mwanadamu hana neno lolote lililo jema chini ya jua, kuliko kula, kunywa, na kujifurahisha; maana hili atakaa nalo katika amali yake, siku zote za maisha yake alizompa Mungu chini ya jua.


Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kuipoteza nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?


Utupe leo riziki yetu.


Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?


Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Maovu ya siku yanaitosha siku hiyo.


Akawaambia wanafunzi wake, Kwa sababu hiyo nawaambia, Msisumbukie maisha yenu, mtakula nini; wala miili yenu, mtavaa nini.


Ninyi msitafute mtakavyokula wala mtakavyokunywa; wala msiwe na wasiwasi,


watiini watu kama hawa, na kila mtu afanyaye kazi pamoja nao, na kujitaabisha.


Msijisumbue kwa neno lolote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.


ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo.


huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo