Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mhubiri 1:3 - Swahili Revised Union Version

3 Mtu ana faida gani ya kazi yake yote aifanyayo chini ya jua?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Binadamu hufaidi nini kwa jasho lake lote hapa duniani?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Binadamu hufaidi nini kwa jasho lake lote hapa duniani?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Binadamu hufaidi nini kwa jasho lake lote hapa duniani?

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Mwanadamu anafaidi nini kutokana na kazi yake yote anayotaabikia chini ya jua?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Mwanadamu anafaidi nini kutokana na kazi yake yote anayotaabikia chini ya jua?

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

3 Mtu ana faida gani ya kazi yake yote aifanyayo chini ya jua?

Tazama sura Nakili




Mhubiri 1:3
23 Marejeleo ya Msalaba  

Kisha nikaziangalia kazi zote zilizofanywa kwa mikono yangu, na taabu yote niliyotaabika katika kuzitenda; na tazama, yote ni ubatili na kufukuza upepo, wala faida hakuna chini ya jua.


Nami nikaichukia kazi yangu yote niliyojishughulisha nayo chini ya jua; maana sina budi kumwachia yeye atakayenifuata.


Naye ni nani ajuaye kama huyo atakuwa mwenye hekima au mpumbavu? Hata hivyo atatawala juu ya kazi yangu yote niliyojishughulisha nayo, ambamo ndani yake mimi nimeonesha hekima chini ya jua. Hayo nayo ni ubatili.


Kwa maana mtu hupata nini kwa kazi yake yote, na kwa juhudi ya moyo wake alivyojitahidi chini ya jua?


Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale anayojishughulisha nayo?


naam, zaidi ya hao wote nikamwita heri yeye asiyekuwako bado, ambaye hakuyaona mabaya yanayotendeka chini ya jua.


Kisha nikarudi tena, na kuona ubatili chini ya jua.


Hiyo ndiyo balaa mbaya sana, ya kwamba kama vile alivyokuja, vivyo hivyo atakwenda zake; naye amefaidiwa nini mwenye kujitaabisha kwa ajili ya upepo?


Tazama, mimi niliyoyaona kuwa ndiyo mema na ya kufaa, ni mtu kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote anayoifanya chini ya jua, siku zote za maisha yake alizopewa na Mungu; maana hilo ndilo fungu lake.


Kwa maana ni nani ajuaye yaliyo mema ya mwanadamu katika maisha yake, siku zote za maisha yake ya ubatili, anayoishi kama kivuli? Kwa maana ni nani awezaye kumweleza mwanadamu mambo yatakayofuata baada yake chini ya jua?


Hekima ni njema kama urithi; Naam, nayo ni bora kwao walionalo jua.


Pia nimeona mfano huu wa hekima chini ya jua, nao ni kama hivi, tena kwangu mimi ulionekana kuwa neno kubwa.


Baa hilo ni katika mambo yote yanayofanyika chini ya jua, ya kuwa wote wanalo tukio moja; naam, zaidi ya hayo, mioyo ya wanadamu imejaa maovu, na wazimu umo mioyoni mwao wakati walipo hai, na baadaye huenda kwa wafu.


Mapenzi yao na chuki yao, na husuda yao, imepotea yote pamoja; wala hawana sehemu tena katika jambo lolote lililofanyika chini ya jua.


Kwa nini mtoe fedha kwa ajili ya kitu ambacho si chakula? Na mapato yenu kwa kitu kisichoshibisha? Nisikilizeni kwa bidii, mle kilicho chema, Na kujifurahisha nafsi zenu kwa unono.


Angalieni; je! Jambo hili halikutoka kwa BWANA wa majeshi, kwamba watu wajishughulikie moto, na mataifa wajisumbue kwa ajili ya ubatili?


Sanamu ya kuchonga yafaa nini, baada ya aliyeifanya ameichonga? Sanamu ya kuyeyuka, nayo ni mwalimu wa uongo, yafaa nini, hata yeye aliyeifanya aiwekee tumaini lake, na kufanya sanamu zisizoweza kusema?


Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kuipoteza nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?


Msikitendee kazi chakula chenye kuharibika, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele; ambacho Mwana wa Adamu atawapa, kwa sababu huyo ndiye aliyetiwa mhuri na Baba, yaani, Mungu.


watiini watu kama hawa, na kila mtu afanyaye kazi pamoja nao, na kujitaabisha.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo