Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 17:23 - Swahili Revised Union Version

23 Asiye haki hutoa rushwa kifuani, Ili kuzipotosha njia za hukumu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

23 Mtu mbaya hupokea hongo kwa siri ili apate kupotosha haki.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

23 Mtu mbaya hupokea hongo kwa siri ili apate kupotosha haki.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

23 Mtu mbaya hupokea hongo kwa siri ili apate kupotosha haki.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

23 Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

23 Asiye haki hutoa rushwa kifuani, Ili kuzipotosha njia za hukumu.

Tazama sura Nakili




Methali 17:23
16 Marejeleo ya Msalaba  

Nawe usipokee rushwa; kwani hiyo rushwa huwapofusha macho hao waonao, na kuyapotoa maneno ya wenye haki.


Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; Kila kigeukapo hufanikiwa.


Zawadi ya mtu humpatia nafasi; Humleta mbele ya watu wakuu.


Kipawa cha siri hutuliza hasira; Na rushwa bindoni humliza ghadhabu kali.


Kweli jeuri humpumbaza mwenye hekima, Na rushwa huuharibu ufahamu.


Wakuu wako ni waasi, na rafiki za wezi; kila mtu hupenda rushwa, hufuata malipo; hawampatii yatima haki yake, wala maneno ya mjane hayawafikii.


wampao haki mwenye uovu, ili wapewe ijara, na kumwondolea mwenye haki haki yake!


Ndani yako wamepokea rushwa ili kumwaga damu; umepokea riba na faida; nawe kwa choyo umepata mapato kwa kuwadhulumu jirani zako, nawe umenisahau mimi, asema Bwana MUNGU.


Wakuu wake kati yake wamekuwa kama mbwamwitu wakirarua mawindo; ili kumwaga damu, na kuharibu roho za watu, wapate faida kwa njia isiyo halali.


Wakuu wake huhukumu ili wapate rushwa, na makuhani wake hufundisha ili wapate ijara, na manabii wake hubashiri ili wapate fedha; ila hata hivyo watamtegemea BWANA, na kusema, Je! Hayupo BWANA katikati yetu? Hapana neno baya lolote litakalotufikia.


Sikieni haya, tafadhali, enyi vichwa vya nyumba ya Yakobo, mnaoitawala nyumba ya Israeli, mnaochukia hukumu, na kuipotosha adili.


Mikono yao ni hodari kwa kutenda maovu; afisa na hakimu wanataka rushwa, mtu mkubwa hunena madhara yaliyomo rohoni mwake; hivyo ndivyo wayafumavyo hayo pamoja.


Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza kesi wa wenye haki.


Nami nipo hapa; basi, mnishuhudie mbele za BWANA, na mbele ya masihi wake, nilitwaa ng'ombe wa nani? Au nilitwaa punda wa nani? Au ni nani niliyemdhulumu? Ni nani niliyemwonea? Au kwa mkono wa nani nimepokea rushwa inipofushe macho? Nami nitawarudishia ninyi.


Ila wanawe hawakuenda katika njia zake, bali waliziacha, ili wapate faida; wakapokea rushwa, na kupotosha hukumu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo