Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Luka 8:31 - Swahili Revised Union Version

31 Wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

31 Hao pepo wakamsihi asiwapeleke kwenye shimo kuu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

31 Hao pepo wakamsihi asiwapeleke kwenye shimo kuu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

31 Hao pepo wakamsihi asiwapeleke kwenye shimo kuu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

31 Wale pepo wachafu wakamsihi sana asiwaamuru kwenda katika Shimo.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

31 Wale pepo wachafu wakamsihi sana asiwaamuru kwenda katika Shimo.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

31 Wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni.

Tazama sura Nakili




Luka 8:31
14 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako.


Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako.


Kisha atawaambia na wale walioko katika mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;


Alipomwona Yesu alipiga kelele, akaanguka mbele yake, akasema kwa sauti kuu, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu? Nakusihi usinitese.


Basi, hapo palikuwa na kundi la nguruwe wengi wakilishwa mlimani; wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale. Akawapa ruhusa.


au, Ni nani atakayeshuka kwenda kuzimuni? (Yaani, ni kumleta Kristo juu, kutoka kwa wafu.)


Hata watakapoumaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika kuzimu atafanya vita nao, naye atawashinda na kuwaua.


Yule mnyama uliyemwona alikuwako, naye hayuko, naye yuko tayari kupanda kutoka kuzimu na kwenda kwenye uharibifu. Na hao wakaao juu ya nchi, wasioandikwa majina yao katika kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, watastaajabu wamwonapo yule mnyama, ya kwamba alikuwako, naye hayuko, naye atakuwako.


Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao hao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wakiwa hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti;


Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu, jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kigiriki analo jina lake Apolioni.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo