Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 60:3 - Swahili Revised Union Version

3 Na mataifa wataijia nuru yako, Na wafalme kuujia mwanga wa mapambazuko yako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Mataifa yataujia mwanga wako, wafalme waujia mwanga wa pambazuko lako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Mataifa yataujia mwanga wako, wafalme waujia mwanga wa pambazuko lako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Mataifa yataujia mwanga wako, wafalme waujia mwanga wa pambazuko lako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Mataifa watakuja kwenye nuru yako na wafalme kwa mwanga wa mapambazuko yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Mataifa watakuja kwenye nuru yako na wafalme kwa mwanga wa mapambazuko yako.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

3 Na mataifa wataijia nuru yako, Na wafalme kuujia mwanga wa mapambazuko yako.

Tazama sura Nakili




Isaya 60:3
43 Marejeleo ya Msalaba  

Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake, Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki, Ambaye mataifa watamtii.


BWANA atakapokuwa ameijenga Sayuni, Atakapoonekana katika utukufu wake,


Pindi mataifa watapokusanyika pamoja, Na falme, ili kumtumikia BWANA.


Ee BWANA, wafalme wote wa dunia watakushukuru, Watakapoyasikia maneno ya kinywa chako.


Na sasa, enyi wafalme, iweni na hekima, Enyi watawala wa dunia, mwaonywa.


Miisho yote ya dunia itakumbuka, Na watu watamrejea BWANA; Jamaa zote za mataifa watamsujudia.


Kwa ajili ya hekalu lako Yerusalemu Wafalme watakuletea hedaya.


Naam, wafalme wote na wamsujudie; Na mataifa yote wamtumikie.


Na itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese lisimamalo kuwa ishara kwa makabila ya watu, yeye ndiye ambaye mataifa watamtafuta; na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu.


Mimi, BWANA, nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono, na kukulinda, na kukutoa uwe agano la watu, na nuru ya mataifa;


BWANA asema hivi, Kazi ya Misri, na bidhaa ya Kushi, na Waseba, watu walio warefu, watakujia, nao watakuwa wako; watakufuata; watakuja katika minyororo; wataanguka chini mbele yako, watakuomba, wakisema, Hakika Mungu yu ndani yako; wala hapana mwingine, hapana Mungu tena.


Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine.


Tazama, hawa watakuja kutoka mbali; na tazama, hawa kutoka kaskazini, na kutoka magharibi, na hawa kutoka nchi ya Sinimu.


Na wafalme watakuwa baba zako walezi, na malkia zao mama zako walezi; watainama mbele yako kifudifudi, na kuramba mavumbi ya miguu yako; nawe utajua ya kuwa mimi ni BWANA, tena waningojeao hawatatahayarika.


Bwana MUNGU, akusanyaye waliofukuzwa katika Israeli asema, Pamoja na hayo nitamkusanyia na wengine, zaidi ya hao walio wake waliokusanywa.


Na wageni watajenga kuta zako, Na wafalme wao watakuhudumu; Maana katika ghadhabu yangu nilikupiga, Lakini katika upendeleo wangu nimekurehemu.


Utanyonya maziwa ya mataifa, Utanyonya matiti ya wafalme; Nawe utajua ya kuwa mimi, BWANA, ni mwokozi wako, Na mkombozi wako, Mwenye enzi wa Yakobo.


Na mataifa wataiona haki yako, na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha BWANA.


Maana BWANA asema hivi, Tazama, nitamwelekezea amani kama mto, na utukufu wa mataifa kama kijito kifurikacho, nanyi mtapata kunyonya; mtabebwa; na juu ya magoti mtabembelezwa.


wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yaitwayo kwa jina langu, asema BWANA, afanyaye hayo.


Na mataifa mengi watajiunga na BWANA katika siku ile, nao watakuwa watu wangu; nami nitakaa kati yako, nawe utajua ya kuwa BWANA wa majeshi amenituma kwako.


Basi, nendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;


na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.


Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu.


Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana, Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, Upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.


Ili wanadamu waliobakia wamtafute Bwana, Na mataifa yote ambao jina langu limetajwa kwao;


Malaika wa saba akapiga baragumu, pakawa na sauti kuu katika mbingu, zikisema, Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atamiliki hata milele na milele.


Na mataifa watatembea katika nuru yake. Na wafalme wa nchi huleta utukufu wao ndani yake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo