Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 59:17 - Swahili Revised Union Version

17 Akajivika haki kama deraya kifuani, na chapeo cha wokovu kichwani pake, akajivika mavazi ya kisasi yawe mavazi yake, naye alivikwa wivu kama joho.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

17 Alivaa uadilifu kama vazi la kujikinga kifuani, na wokovu kama kofia ya chuma kichwani. Atajivika kisasi kama vazi, na kujifunika wivu kama joho.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

17 Alivaa uadilifu kama vazi la kujikinga kifuani, na wokovu kama kofia ya chuma kichwani. Atajivika kisasi kama vazi, na kujifunika wivu kama joho.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

17 Alivaa uadilifu kama vazi la kujikinga kifuani, na wokovu kama kofia ya chuma kichwani. Atajivika kisasi kama vazi, na kujifunika wivu kama joho.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

17 Alivaa haki kama dirii kifuani mwake, na chapeo ya wokovu kichwani mwake, alivaa mavazi ya kisasi naye akajifunga wivu kama joho.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

17 Alivaa haki kama dirii kifuani mwake, na chapeo ya wokovu kichwani mwake, alivaa mavazi ya kisasi naye akajifunga wivu kama joho.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

17 Akajivika haki kama deraya kifuani, na chapeo cha wokovu kichwani pake, akajivika mavazi ya kisasi yawe mavazi yake, naye alivikwa wivu kama joho.

Tazama sura Nakili




Isaya 59:17
24 Marejeleo ya Msalaba  

Nilijivika haki, ikanifunika, Adili yangu ilikuwa kama joho na kilemba.


Maana mvuto wa nyumba yako umenila, Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata.


Ee BWANA, Mungu wa kisasi, Mungu wa kisasi, uangaze,


Na haki itakuwa mshipi wa viuno vyake, na uaminifu mshipi wa kujifungia.


BWANA, mkono wako umeinuliwa, lakini hawaoni; lakini watauona wivu wako kwa ajili ya watu wako, nao watatahayari; naam, moto utawala adui zako.


Maana katika Yerusalemu yatatoka mabaki, nao watakaookoka katika mlima Sayuni; wivu wa BWANA wa majeshi utatimiza mambo hayo.


BWANA atatokea kama shujaa; Ataamsha wivu kama mtu wa vita; Atalia, naam, atapiga kelele; Atawatenda adui zake mambo makuu.


Amka, amka, jivike nguvu, Ee mkono wa Bwana; Amka kama katika siku zile za kale, Katika vizazi vile vya zamani.


Tazama toka mbinguni, ukaone toka makao ya utukufu wako na fahari yako; uko wapi wivu wako, na uweza wako? Shauku ya moyo wako, na huruma zako zimezuiliwa kwangu.


Kwa nini mavazi yako ni mekundu, Na nguo zako kama za mtu akanyagaye zabibu?


Nilikanyaga shinikizoni peke yangu; Wala katika watu hakuwapo mtu pamoja nami; Naam, niliwakanyaga kwa hasira yangu, Niliwaponda kwa ghadhabu yangu; Na mavazi yangu yametiwa madoa kwa damu yao, Nami nimezichafua nguo zangu zote.


Mamlaka ya enzi yake yatakuzwa daima, Na kutakuwa na amani isiyo na mwisho, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa BWANA wa majeshi ndio utakaotenda hayo.


Hivyo ndivyo ghadhabu yangu itakavyotimia, nami nitatosheleza hasira yangu juu yao, nami nitafarijika; nao watajua ya kuwa mimi, BWANA, nimenena kwa wivu wangu, nitakapokuwa nimeitimiza ghadhabu yangu juu yao.


Basi yule malaika aliyesema nami akaniambia, Haya, piga kelele na kusema, BWANA wa majeshi asema hivi, Naona wivu kwa ajili ya Yerusalemu, na kwa ajili ya Sayuni; naona wivu mkuu sana.


Wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa imeandikwa, Wivu wa nyumba yako utanila.


katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu; kwa silaha za haki za mkono wa kulia na za mkono wa kushoto;


Basi simameni, mkiwa mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,


Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;


Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.


katika muali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu;


Maana twamjua yeye aliyesema, Kupatiliza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipa. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake.


Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo