Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 57:7 - Swahili Revised Union Version

7 Umeweka kitanda chako juu ya mlima mrefu ulioinuka sana; ukaenda huko ili kutoa dhabihu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Mmeweka vitanda vyenu juu ya milima mikubwa, na kwenda huko kutoa tambiko.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Mmeweka vitanda vyenu juu ya milima mikubwa, na kwenda huko kutoa tambiko.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Mmeweka vitanda vyenu juu ya milima mikubwa, na kwenda huko kutoa tambiko.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Umeweka kitanda chako juu kwenye kilima kirefu kilichoinuka, huko ulienda kutoa dhabihu zako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Umeweka kitanda chako juu kwenye kilima kirefu kilichoinuka, huko ulikwenda kutoa dhabihu zako.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

7 Umeweka kitanda chako juu ya mlima mrefu ulioinuka sana; ukaenda huko ili kutoa dhabihu.

Tazama sura Nakili




Isaya 57:7
12 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini ninyi karibuni hapa, enyi wana wa mwanamke mchawi, uzao wa mzinzi na kahaba.


maovu yenu na maovu ya baba zenu pamoja, asema BWANA, ninyi mliofukiza uvumba juu ya milima, na kunitukana juu ya vilima; basi, kwa ajili ya hayo nitawapimia kwanza kazi yao vifuani mwao.


Kwa maana tangu zamani wewe umeivunja nira yako, na kuvipasua vifungo vyako; ukasema, Mimi sitatumika; kwa maana juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti wenye majani mabichi, umejiinamisha, ukafanya mambo ya ukahaba.


Inua macho yako, ukavitazame vilele vya milima, ukaone; pako wapi mahali ambapo hawakulala nawe? Kando ya njia umeketi ili kuwangojea, kama vile Mwarabu jangwani; nawe umeitia nchi unajisi kwa ukahaba wako na uovu wako.


Tena, BWANA akaniambia siku za mfalme Yosia, Je! Umeyaona aliyotenda Israeli mwenye kuasi? Amepanda juu ya kila mlima mrefu, akafanya huko mambo ya ukahaba, tena, chini ya kila mti wenye majani mabichi.


Ukatwaa baadhi ya mavazi yako, ukajifanyia mahali palipoinuka, palipopambwa kwa rangi mbalimbali, ukafanya mambo ya kikahaba juu yake; mambo kama hayo hayatakuja wala hayatakuwako.


ulijijengea mahali palipoinuka, ukajifanyia mahali palipoinuka katika kila njia kuu.


Umejenga mahali pako palipoinuka penye kichwa cha kila njia, ukaufanya uzuri wako kuwa chukizo, ukatanua miguu yako kwa kila mtu aliyepita karibu, ukaongeza mambo yako ya kikahaba.


Na watu wa Babeli wakamwendea katika kitanda cha mapenzi, wakamtia unajisi kwa uzinzi wao, akatiwa unajisi nao, kisha roho yake ikafarakana nao.


ukaketi juu ya kitanda cha enzi, na meza imeandikwa tayari mbele yake, ambayo juu yake uliweka uvumba wangu na mafuta yangu.


Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, watu wa kwao waliouawa watakapokuwa kati ya vinyago vyao, pande zote za madhabahu zao, juu ya kila kilima kirefu, juu ya vilele vya milima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi, na chini ya kila mwaloni mnene, pale pale walipovifukizia uvumba mzuri vinyago vyao vyote.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo