Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 5:27 - Swahili Revised Union Version

27 Miongoni mwao hakuna achokaye wala kukwaa; Hakuna asinziaye wala kulala usingizi; Wala mshipi wa viuno vyao hautalegea. Wala ukanda wa viatu vyao hautakatika;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

27 Hawachoki wala hawajikwai; hawasinzii wala hawalali; hakuna mshipi wao uliolegea wala kamba ya kiatu iliyokatika.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

27 Hawachoki wala hawajikwai; hawasinzii wala hawalali; hakuna mshipi wao uliolegea wala kamba ya kiatu iliyokatika.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

27 Hawachoki wala hawajikwai; hawasinzii wala hawalali; hakuna mshipi wao uliolegea wala kamba ya kiatu iliyokatika.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

27 Hakuna hata mmoja wao anayechoka wala kujikwaa, hakuna hata mmoja anayesinzia wala kulala, hakuna mkanda uliolegezwa kiunoni, hakuna gidamu ya kiatu iliyokatika.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

27 Hakuna hata mmoja wao anayechoka wala kujikwaa, hakuna hata mmoja anayesinzia wala kulala, hakuna mkanda uliolegezwa kiunoni, hakuna gidamu ya kiatu iliyokatika.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

27 Miongoni mwao hakuna achokaye wala kujikwaa; Hakuna asinziaye wala kulala usingizi; Wala mshipi wa viuno vyao hautalegea. Wala ukanda wa viatu vyao hautakatika;

Tazama sura Nakili




Isaya 5:27
14 Marejeleo ya Msalaba  

Na zaidi ya hayo, unajua alivyonitenda Yoabu, mwana wa Seruya, yaani, alivyowatenda majemadari wawili wa majeshi ya Israeli, Abneri, mwana wa Neri, na Amasa, mwana wa Yetheri, ambao aliwaua, na kumwaga damu wakati wa amani akilipiza kisasi cha vita, mshipi akautia damu ya vita uliokuwa viunoni mwake, na viatu vilivyokuwa miguuni mwake.


Yeye hulegeza kifungo cha wafalme, Na kuwafunga viuno vyao kwa mshipi.


Humwaga aibu juu ya hao wakuu, Na kulegeza mshipi wa wenye nguvu.


Mungu ndiye anifungaye mshipi wa nguvu, Naye anaifanya kamilifu njia yangu.


BWANA ametamalaki, amejivika adhama, BWANA amejivika, ukuu na nguvu, kama mavazi ya kifalme. Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;


Ndipo utakapokwenda katika njia yako salama, Wala mguu wako hautakwaa.


Na haki itakuwa mshipi wa viuno vyake, na uaminifu mshipi wa kujifungia.


Haya ndiyo BWANA amwambiayo Koreshi, masihi wake, ambaye nimemshika mkono wake wa kulia, ili kutiisha mataifa mbele yake, nami nitalegeza nguvu za wafalme; ili kufungua milango mbele yake, hata malango hayatafungwa.


Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine; zaidi yangu mimi hapana Mungu; nitakuimarisha ijapokuwa hukunijua;


Ndipo uso wa mfalme ukambadilika; fikira zake zikamfadhaisha; viungo vya viuno vyake vikalegea; magoti yake yakagongana.


Naye Yohana mwenyewe alikuwa na vazi lake la singa za ngamia, na mshipi wa ngozi kiunoni mwake; na chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.


Nje upanga utawafifiliza Na ndani ya vyumba, utisho; Utaangamiza mvulana na msichana, Anyonyaye pamoja na mwenye mvi,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo