Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 45:25 - Swahili Revised Union Version

25 Katika BWANA wazao wote wa Israeli watapewa haki, na kutukuka.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

25 Lakini wazawa wa Israeli watapata ushindi kwake Mwenyezi-Mungu na kufurahi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

25 Lakini wazawa wa Israeli watapata ushindi kwake Mwenyezi-Mungu na kufurahi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

25 Lakini wazawa wa Israeli watapata ushindi kwake Mwenyezi-Mungu na kufurahi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

25 Lakini katika Mwenyezi Mungu wazao wote wa Israeli wataonekana wenye haki na watashangilia.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

25 Lakini katika bwana wazao wote wa Israeli wataonekana wenye haki na watashangilia.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

25 Katika BWANA wazao wote wa Israeli watapewa haki, na kutukuka.

Tazama sura Nakili




Isaya 45:25
36 Marejeleo ya Msalaba  

basi, usikie huko mbinguni, ukatende, ukawahukumu watumwa wako; ukimpatiliza mtu mbaya, kwa kuleta njia yake juu ya kichwa chake; na kumpa mwenye haki haki yake, ukimjalia kwa kadiri ya haki yake.


Enyi wazao wa Israeli, mtumishi wake, Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.


Ninyi mnaomcha BWANA, msifuni, Enyi nyote mlio wazawa wa Yakobo, mtukuzeni, Mcheni, enyi nyote mlio wazawa wa Israeli.


Mwenye haki atamfurahia BWANA na kumkimbilia, Na wote wenye moyo wa adili watasifu.


Fungueni malango yake, Taifa lenye haki, lishikalo kweli, liingie.


Katika siku ile BWANA wa majeshi atakuwa ni taji la fahari, na kilemba cha uzuri, kwa mabaki ya watu wake.


Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia BWANA, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli.


Bali Israeli wataokolewa na BWANA kwa wokovu wa milele; ninyi hamtatahayarika, wala kufadhaika, milele na milele.


Sikusema kwa siri, katika mahali pa nchi ya giza; sikuwaambia wazao wa Yakobo; Nitafuteni bure; Mimi, BWANA, nasema ukweli; nanena mambo ya haki.


Mmoja ataniambia, Kwa BWANA, peke yake, iko haki na nguvu; naam, watu watamwendea yeye, na wote waliomkasirikia watatahayarika.


Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu; ni nani atakayeshindana nami? Na tusimame pamoja; ni nani aliye hasimu yangu? Na anikaribie basi.


Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki Atawafanya wengi kuwa wenye haki; Naye atayachukua maovu yao.


Jua halitakuwa nuru yako tena wakati wa mchana, Wala mwezi hautakupa nuru kwa mwangaza wake; Bali BWANA atakuwa nuru ya milele kwako, Na Mungu wako atakuwa utukufu wako.


Watu wako nao watakuwa wenye haki wote, Nao watairithi nchi milele; Wao ni chipukizi nililolipanda mimi mwenyewe, Kazi ya mikono yangu mwenyewe, Ili mimi nitukuzwe.


Na kizazi chao kitajulikana katika mataifa, na uzao wao katika makabila ya watu; wote wawaonao watakiri ya kuwa wao ni kizazi kilichobarikiwa na BWANA.


Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa kwa taabu; kwa sababu wao ni wazao wa hao waliobarikiwa na BWANA, na watoto wao pamoja nao.


Nami nitaleta uzao toka Yakobo, na mrithi wa milima yangu toka Yuda, na mteule wangu atairithi, na watumishi wangu watakaa huko.


Katika siku zile Yuda ataokolewa, na Yerusalemu utakaa salama, na jina lake atakaloitwa ni hili, BWANA ni haki yetu.


nawe utaapa hivi, Kama BWANA aishivyo, katika kweli, na katika hukumu, na katika haki ndipo mataifa watabarikiwa na yeye, nao watajitukuza katika yeye.


na kwa yeye kila amwaminiye huhesabiwa haki katika mambo yale yote asiyoweza kuhesabiwa haki kwa Torati ya Musa.


Kwa hiyo ilitoka katika imani, iwe kwa njia ya neema, ili kwamba ile ahadi iwe imara kwa wazawa wote; si kwa wale wa torati tu, ila na kwa wale wa imani ya Abrahamu; aliye baba yetu sisi sote;


Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na muwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,


Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.


Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza.


kusudi, kama ilivyoandikwa, Yeye aonaye fahari na aone fahari juu ya Bwana.


Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.


Lakini, Yeye ajisifuye, na ajisifu katika Bwana.


Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye.


Lakini mimi, la hasha, nisione fahari juu ya kitu chochote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulubishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu.


Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo