Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 43:26 - Swahili Revised Union Version

26 Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

26 “Niambie kama mna kisa nami, njoo tukahojiane; toeni mashtaka yenu ili tuuone ukweli wenu!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

26 “Niambie kama mna kisa nami, njoo tukahojiane; toeni mashtaka yenu ili tuuone ukweli wenu!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

26 “Niambie kama mna kisa nami, njoo tukahojiane; toeni mashtaka yenu ili tuuone ukweli wenu!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, jitetee uweze kupewa haki yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

26 Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako.

Tazama sura Nakili




Isaya 43:26
19 Marejeleo ya Msalaba  

Nawe ulisema, Hakika nitakutendea mema, nami nitafanya uzao wako uwe kama mchanga wa bahari, usiohesabika kwa kuwa mwingi.


Laiti angemtolea mtu hoja mbele ya Mungu, Amtetee na mwanadamu mbele ya jirani yake.


Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.


Ee Mungu, usimame, ujitetee mwenyewe, Ukumbuke unavyotukanwa na mpumbavu mchana kutwa.


Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama damu, zitakuwa kama sufu.


Nyamazeni mbele zangu, enyi visiwa, na mataifa wajipatie nguvu mpya; na waje karibu wakanene; na tukaribiane pamoja kwa hukumu.


Na wakusanyike mataifa yote, kabila zote wakutanike; ni nani miongoni mwao awezaye kuhubiri neno hili, na kutuonesha mambo ya zamani? Na walete mashahidi wao, wapate kuhesabiwa kuwa na haki; au na wasikie, wakaseme, Ni kweli.


Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu; ni nani atakayeshindana nami? Na tusimame pamoja; ni nani aliye hasimu yangu? Na anikaribie basi.


Bwana MUNGU asema hivi, Tena kwa ajili ya jambo hili nitaulizwa na nyumba ya Israeli, ili niwatendee; nami nitawaongeza kwa watu kama kundi la kondoo.


Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani?


Akawaambia, Ninyi ndinyi mnaojidai haki mbele ya wanadamu, lakini Mungu awajua mioyo yenu; kwa kuwa lililotukuka kwa wanadamu huwa chukizo mbele za Mungu.


Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.


Au ni nani aliyempa yeye kitu kwanza, naye atalipwa tena?


Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo