Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 28:10 - Swahili Revised Union Version

10 Kwa maana ni amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Anatufundisha kama watoto wadogo: Sheria baada ya sheria, mstari baada ya mstari; mara hiki, mara kile!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Anatufundisha kama watoto wadogo: Sheria baada ya sheria, mstari baada ya mstari; mara hiki, mara kile!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Anatufundisha kama watoto wadogo: sheria baada ya sheria, mstari baada ya mstari; mara hiki, mara kile!”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Kwa maana ni: Amri juu ya amri, amri juu ya amri, kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; hapa kidogo, kule kidogo.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Kwa maana ni: Amri juu ya amri, amri juu ya amri, kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; hapa kidogo, kule kidogo.”

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

10 Kwa maana ni amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo.

Tazama sura Nakili




Isaya 28:10
11 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo; ili waende na kuanguka nyuma, na kuvunjwa, na kunaswa, na kuchukuliwa.


Je! Ni kazi gani iliyohitajika kutendeka ndani ya shamba langu la mizabibu nisiyoitenda? Basi, nilipotumaini ya kuwa litazaa zabibu, mbona lilizaa zabibumwitu?


Kwa maana niliwashuhudia sana baba zenu, siku ile nilipowatoa katika nchi ya Misri, hata leo, nikiamka mapema na kuwashuhudia, nikisema, Itiini sauti yangu.


Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana. Kuwaandikieni mambo yale yale hakuniudhi mimi, bali kutawafaa ninyi.


wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.


Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo