Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 26:2 - Swahili Revised Union Version

2 Fungueni malango yake, Taifa lenye haki, lishikalo kweli, liingie.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 Fungueni malango ya mji, taifa aminifu liingie; taifa litendalo mambo ya haki.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 Fungueni malango ya mji, taifa aminifu liingie; taifa litendalo mambo ya haki.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 Fungueni malango ya mji, taifa aminifu liingie; taifa litendalo mambo ya haki.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 Fungua malango ili taifa lenye haki lipate kuingia, taifa lidumishalo imani.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 Fungua malango ili taifa lenye haki lipate kuingia, taifa lile lidumishalo imani.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

2 Fungueni malango yake, Taifa lenye haki, lishikalo kweli, liingie.

Tazama sura Nakili




Isaya 26:2
25 Marejeleo ya Msalaba  

Ili niuone wema wa wateule wako. Nipate kuifurahia furaha ya taifa lako, Na kujisifu pamoja na watu wako.


Nifungulieni malango ya haki, Nitaingia na kumshukuru BWANA.


Lango hili ni la BWANA, Wenye haki ndio watakaoliingia.


Inueni vichwa vyenu, enyi malango, Inukeni, enyi malango ya milele, Mfalme wa utukufu apate kuingia.


nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu. Hayo ndiyo maneno utakayowaambia wana wa Israeli.


Katika BWANA wazao wote wa Israeli watapewa haki, na kutukuka.


Utathibitika katika haki; utakuwa mbali na kuonewa, kwa maana hutaogopa; na mbali na hofu, kwa maana haitakukaribia.


Kila silaha itengenezwayo juu yako haitafanikiwa, na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa BWANA, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema BWANA.


Ndipo nuru yako itakapopambazuka kama asubuhi, na uponyaji wako utatokea punde; na haki yako itakutangulia; utukufu wa BWANA utakufuata nyuma ukulinde.


Malango yako nayo yatakuwa wazi daima; Hayatafungwa mchana wala usiku; Ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa, Huku wakiwaongoza wafalme wao.


Jeuri haitasikiwa tena katika nchi yako, Ukiwa na uharibifu hazitakuwa mipakani mwako; Bali utaziita kuta zako, Wokovu, Na malango yako, Sifa.


Watu wako nao watakuwa wenye haki wote, Nao watairithi nchi milele; Wao ni chipukizi nililolipanda mimi mwenyewe, Kazi ya mikono yangu mwenyewe, Ili mimi nitukuzwe.


kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji la maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na BWANA, ili atukuzwe.


Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia, hata haki yake itakapotokea kama mwangaza, na wokovu wake kama taa iwakayo.


Piteni, piteni, katika malango; Itengenezeni njia ya watu; Tutieni, tutieni barabara; toeni mawe yake; Twekeni bendera kwa ajili ya makabila ya watu.


Na mataifa wataiona haki yako, na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha BWANA.


BWANA wa majeshi asema hivi, Baadaye watakuja mataifa na wenyeji wa miji mingi;


wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.


Bali ninyi ni uzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;


Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.


Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, niliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu.


Na mataifa watatembea katika nuru yake. Na wafalme wa nchi huleta utukufu wao ndani yake.


Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuifungua mihuri yake; kwa kuwa ulichinjwa, ukawa fidia kwa Mungu na kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo