Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 26:14 - Swahili Revised Union Version

14 Wao wamekufa, hawataishi; wamekwisha kufariki, hawatafufuka; kwa sababu hiyo umewajia, na kuwaangamiza, na kuupoteza ukumbusho wao.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

14 Watu hao wamekufa, wala hawataishi tena; wamekuwa mizimu, wala hawatafufuka. Maana wewe umewaadhibu na kuwaangamiza, hakuna atakayeweza kuwakumbuka tena.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

14 Watu hao wamekufa, wala hawataishi tena; wamekuwa mizimu, wala hawatafufuka. Maana wewe umewaadhibu na kuwaangamiza, hakuna atakayeweza kuwakumbuka tena.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

14 Watu hao wamekufa, wala hawataishi tena; wamekuwa mizimu, wala hawatafufuka. Maana wewe umewaadhibu na kuwaangamiza, hakuna atakayeweza kuwakumbuka tena.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

14 Wao sasa wamekufa, wala hawako tena hai, roho za waliokufa hazitarudi tena. Uliwaadhibu na kuwaangamiza, umefuta kumbukumbu lao lote.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

14 Wao sasa wamekufa, wala hawako tena hai, roho za waliokufa hazitarudi tena. Uliwaadhibu na kuwaangamiza, umefuta kumbukumbu lao lote.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

14 Wao wamekufa, hawataishi; wamekwisha kufariki, hawatafufuka; kwa sababu hiyo umewajia, na kuwaangamiza, na kuupoteza ukumbusho wao.

Tazama sura Nakili




Isaya 26:14
25 Marejeleo ya Msalaba  

Kumbukumbu lake litakoma katika nchi, Wala hatakuwa na jina mashambani.


Tumbo lililomzaa litamsahau; buu litamla na kuona tamu; Hatakumbukwa tena; Na udhalimu utavunjwa kama mti.


Kama vile wingu likomavyo na kutoweka, Ndivyo alivyo huyo ashukaye kuzimuni, hatazuka tena kabisa.


Wakamwabudu Baal-Peori, Wakazila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.


Wazawa wake waangamizwe, Jina lao likafutwe katika kizazi cha pili.


Zina masikio lakini hazisikii, Wala hamna pumzi vinywani mwake.


Huko ndiko walikoanguka wafanyao maovu; Wameangushwa chini wasiweze kusimama.


Na Wewe, BWANA, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, uinuke. Uwapatilize mataifa yote; Usimrehemu hata mmoja wa wale wapangao maovu kwa hila.


Adui wameangamia na kuwa magofu milele. Nayo miji yao uliing'oa; Hata kumbukumbu lao limepotea.


Ndivyo BWANA alivyowaokoa Israeli siku ile mikononi mwa Wamisri; Waisraeli wakawaona Wamisri ufuoni mwa bahari, wamekufa.


Kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka; Bali jina la mtu mwovu litaoza.


kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lolote, wala hawana tuzo tena; maana hata kumbukumbu lao limesahauliwa.


Nanyi mtafanya nini siku ya kujiliwa, na wakati wa uangamivu, utakaokuja kutoka mbali sana? Je! Mtamkimbilia nani mpate msaada? Na utukufu wenu mtauacha wapi?


Wafu wako wataishi, maiti zangu zitafufuka; amkeni, kaimbeni, ninyi mnaokaa mavumbini, kwa maana umande wako ni kama umande wa mimea, nayo ardhi itawatoa waliokufa.


Naye atajiliwa na BWANA wa majeshi kwa ngurumo, na tetemeko la nchi, na sauti kuu, na chamchela, na tufani, na mwali wa moto uteketezao.


na kuwatupa miungu yao motoni; kwa maana hao hawakuwa miungu, bali kazi ya mikono ya wanadamu; walikuwa miti na mawe, ndiyo sababu wakawaharibu.


Na wakati watakapokuambia, Tafuta habari kwa watu wenye pepo na kwa wachawi; waliao kama ndege na kunong'ona; je! Haiwapasi watu kutafuta habari kwa Mungu wao? Je! Waende kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?


akasema, Inuka, umchukue mtoto na mamaye, ushike njia kwenda nchi ya Israeli; kwa maana wamekufa walioitafuta roho ya mtoto.


Na huko mtatumikia miungu, waliotengenezwa kwa mikono ya watu, miti na mawe, miungu ambao hawaoni, hawasikii, hawali, wala hawanusi.


Hao wafu waliobakia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo