Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 17:13 - Swahili Revised Union Version

13 Mataifa wananguruma kama ngurumo ya maji mengi; Lakini atawakemea, nao watakimbia mbali sana, Watafukuzwa kama makapi milimani mbele ya upepo, Na kama mavumbi vuruvuru mbele ya tufani.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

13 Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi, lakini Mungu atayakemea, nayo yatakimbilia mbali. Yatafukuzwa kama makapi mlimani mbele ya upepo; kama vumbi litimuliwalo na kimbunga.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

13 Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi, lakini Mungu atayakemea, nayo yatakimbilia mbali. Yatafukuzwa kama makapi mlimani mbele ya upepo; kama vumbi litimuliwalo na kimbunga.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

13 Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi, lakini Mungu atayakemea, nayo yatakimbilia mbali. Yatafukuzwa kama makapi mlimani mbele ya upepo; kama vumbi litimuliwalo na kimbunga.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

13 Ingawa mataifa yanavuma kama ngurumo za maji yanayofanya mawimbi, wakati anayakemea yanakimbia mbali, yanafukuzwa mbele ya upepo kama makapi juu ya milima, kama jani likivingirishwa na dhoruba.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

13 Ingawa mataifa yanavuma kama ngurumo za maji yanayofanya mawimbi, wakati anapoyakemea yanakimbia mbali, yanafukuzwa mbele ya upepo kama makapi juu ya milima, kama jani livingirishwapo na dhoruba.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

13 Mataifa wananguruma kama ngurumo ya maji mengi; Lakini atawakemea, nao watakimbia mbali sana, Watafukuzwa kama makapi milimani mbele ya upepo, Na kama mavumbi vuruvuru mbele ya tufani.

Tazama sura Nakili




Isaya 17:13
33 Marejeleo ya Msalaba  

Ili wawe kama mabua makavu mbele ya upepo, Kama makapi yaliyochukuliwa na dhoruba?


Nikasema, Utafika mpaka hapa, lakini hutapita, Na hapa mawimbi yako yenye nguvu yatazuiliwa?


Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.


Wawe kama makapi mbele ya upepo, Malaika wa BWANA akiwaangusha chini.


Watuliza kuvuma kwa bahari, Kuvuma kwa mawimbi yake, Na ghasia za watu;


Kwa hiyo wakaao mbali kabisa huogopa ishara zako; Milango ya asubuhi na jioni waifurahisha.


Umewakemea mataifa; Na kumwangamiza mdhalimu; Umelifuta jina lao milele na milele;


kwamba nitamvunja huyo Mwashuri vipande vipande katika nchi yangu, na juu ya mlima wangu nitamkanyaga chini ya miguu yangu; ndipo nira yake iliyo juu yao itakapoondoka, na mzigo wake utatoka mabegani mwao.


Kwa maana wanakimbia mbele ya panga, Upanga uliofutwa, na upinde uliopindwa, Na mbele ya ukali wa vita.


Hakika atakukunja na kukutupa kama mpira, mpaka nchi iliyo mbali; huko utakufa, na magari ya utukufu wako yatakuwa kuko huko, ewe uliye aibu ya nyumba ya bwana wako.


Katika siku hiyo BWANA, kwa upanga wake ulio mkali, ulio mkubwa, ulio na nguvu, atamwadhibu Lewiathani, nyoka yule mwepesi, na Lewiathani, nyoka yule mwenye kuzongazonga; naye atamwua yule joka aliye baharini.


Lakini wingi wa adui zako utakuwa kama mavumbi laini, na wingi wao watishao utakuwa kama makapi yapitayo; naam, itakuwa mara na kwa ghafla.


na pumzi yake ni kijito kifurikacho, kifikacho hata shingoni, kupepeta mataifa kwa ungo wa ubatili; na lijamu ikoseshayo itakuwa katika taya za watu.


Naye amewapigia kura, na mkono wake umewagawanyia kwa kamba; wataimiliki hata milele, watakaa ndani yake kizazi hata kizazi.


Tazama, mataifa ni kama tone la maji katika ndoo, huhesabiwa kuwa kama mavumbi membamba katika mizani; tazama, yeye huvinyanyua visiwa kama ni kitu kidogo sana.


Naam, hawakupandwa; hawakutiwa katika ardhi kama mbegu; naam, shina lao halikutia mizizi katika ardhi; tena awapuzia tu, wakanyauka, upepo wa kisulisuli wawaondoa kama mabua makavu.


Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia.


basi sasa angalia; Bwana aleta juu yao maji ya huo Mto, yenye nguvu, mengi sana, nayo ni mfalme wa Ashuru na utukufu wake wote; naye atakuja, na kupita juu ya mifereji yake yote, atafurika juu ya kingo zake zote;


Ndipo kile chuma, na ule udongo, na ile shaba, na ile fedha, na ile dhahabu, vilivunjwa vipande vipande pamoja vikawa kama makapi ya viwanja vya kupepetea wakati wa joto; upepo ukavipeperusha hata pasionekane mahali pake; na lile jiwe lililoipiga hiyo sanamu likawa milima mikubwa, likaijaza dunia yote.


Kwa sababu hiyo watakuwa kama wingu la asubuhi, na kama umande utowekao upesi, kama makapi yaliyopeperushwa na tufani sakafuni, na kama moshi utokao katika bomba.


kabla haijatolewa hiyo amri, kabla siku ile haijapita kama makapi, kabla haijawajia hasira kali ya BWANA, kabla haijawajia siku ya hasira ya BWANA.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo