Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Hesabu 6:26 - Swahili Revised Union Version

26 BWANA akuinulie uso wake, na kukupa amani.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

26 Mwenyezi-Mungu awaoneshe wema wake na kuwapa amani.’

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

26 Mwenyezi-Mungu awaoneshe wema wake na kuwapa amani.’

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

26 Mwenyezi-Mungu awaoneshe wema wake na kuwapa amani.’

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

26 Mwenyezi Mungu akugeuzie uso wake na kukupa amani.” ’

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

26 bwana akugeuzie uso wake na kukupa amani.” ’

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

26 BWANA akuinulie uso wake, na kukupa amani.

Tazama sura Nakili




Hesabu 6:26
24 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA na awape watu wake nguvu; BWANA na awabariki watu wake kwa amani.


Umwangalie sana mtu mkamilifu, Umtazame mtu mnyofu, Maana mwisho wake mtu huyo ni amani.


Wengi husema, Nani atakayetuonesha mema? BWANA, utuinulie nuru ya uso wako.


Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumainie Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.


Maana hawakuitwaa nchi kwa upanga wao, Wala hawakupata ushindi kwa mkono wao; Bali mkono wako wa kulia, naam, mkono wako, Na nuru ya uso wako, kwa kuwa ulipendezwa nao.


Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe, Ee BWANA, waendao, katika nuru ya uso wako.


BWANA, utatuamuria amani; maana ni wewe pia uliyetutendea kazi zetu zote.


Utamlinda yeye ambaye moyo wake umekutegemea Katika amani kamilifu, kwa kuwa anakutumaini.


Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; asema BWANA; nami nitamponya.


Na mtu huyu atakuwa amani yetu; wakati Mwashuri atakapoingia katika nchi yetu, na kuyakanyaga majumba yetu, hapo mtawaleta wachungaji saba juu yake, na wakuu wanane.


Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.


Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.


Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.


Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawatuma ninyi.


Basi, baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwamo ndani tena, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu, na milango imefungwa, akasimama katikati, akasema, Amani iwe kwenu.


Neno lile alilowapelekea wana wa Israeli akihubiri Habari Njema ya amani kwa Yesu Kristo (ndiye Bwana wa wote),


Umenijulisha njia za uzima; Utanijaza furaha kwa uso wako.


Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mtakatifu.


Mungu wa amani na awe pamoja nanyi nyote. Amina.


Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na muwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,


Amani na iwe kwa ndugu, na upendo, pamoja na imani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Bwana Yesu Kristo.


Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.


Sasa, Bwana wa amani mwenyewe na awape amani daima kwa njia zote. Bwana awe pamoja nanyi nyote.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo