Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Hesabu 6:23 - Swahili Revised Union Version

23 Nena na Haruni na wanawe, uwaambie, Hivi ndivyo mtakavyowabariki wana wa Israeli; mtawaambia;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

23 “Mwambie Aroni na wanawe kwamba hivi ndivyo mtakavyowabariki Waisraeli: Mtawaambia,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

23 “Mwambie Aroni na wanawe kwamba hivi ndivyo mtakavyowabariki Waisraeli: Mtawaambia,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

23 “Mwambie Aroni na wanawe kwamba hivi ndivyo mtakavyowabariki Waisraeli: Mtawaambia,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

23 “Mwambie Haruni na wanawe, ‘Hivi ndivyo mtakavyowabariki Waisraeli. Waambieni:

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

23 “Mwambie Haruni na wanawe, ‘Hivi ndivyo mtakavyowabariki Waisraeli. Waambieni:

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

23 Nena na Haruni na wanawe, uwaambie, Hivi ndivyo mtakavyowabariki wana wa Israeli; mtawaambia;

Tazama sura Nakili




Hesabu 6:23
27 Marejeleo ya Msalaba  

Wakambariki Rebeka, wakamwambia, Dada yetu, wewe uwe mama wa elfu kumi, mara elfu nyingi, na wazao wako waurithi mlango wa hao wawachukiao.


Yakobo akambariki Farao, akatoka mbele ya Farao.


Yusufu akamleta Yakobo babaye ndani akamweka mbele ya Farao, Yakobo akambariki Farao.


Akawabariki siku ile akisema, Katika ninyi Waisraeli watabariki, wakisema, Mungu na akufanye kama Efraimu na kama Manase. Akamweka Efraimu mbele ya Manase.


Akasimama, na kuwabariki mkutano wote wa Israeli kwa sauti kuu, akasema,


Wana wa Amramu; Haruni na Musa; naye Haruni akatengwa, ili ayatakase yaliyo matakatifu sana, yeye na wanawe milele, ili kufukiza uvumba mbele za BWANA, kumtumikia, na kubariki kwa jina lake, milele.


Ndipo wakasimama makuhani Walawi, wakawabariki watu; ikasikiwa sauti yao, sala yao ikafika hata makao yake matakatifu, yaani, mbinguni.


Musa akaiona hiyo kazi yote, na tazama, walikuwa wameimaliza; vile vile kama BWANA alivyoagiza, walikuwa wameifanya vivyo hivyo; basi Musa akawaombea heri.


Kisha BWANA akanena na Musa, na kumwambia,


kwa wote walioko Rumi, wapendwao na Mungu, walioitwa kuwa watakatifu. Neema na iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.


Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.


Na wakati huo BWANA alilitenga kabila la Lawi ili walichukue lile sanduku la Agano la BWANA, wasimame mbele ya BWANA kwa kumtumikia, na kuwabarikia watu kwa jina lake, hata hivi leo.


nao makuhani wana wa Lawi wasongee karibu, kwa kuwa ndio aliowachagua BWANA, Mungu wako, wamtumikie, na kubariki katika jina la BWANA na kila neno lishindaniwalo, na kila pigo, litakuwa kwa kufuata maneno yao;


Hii ndiyo baraka ya Musa, huyo mtu wa Mungu, aliyowabarikia wana wa Israeli kabla ya kufa kwake.


Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Abrahamu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki;


Wala haikanushiki kabisa kwamba mdogo hubarikiwa na mkubwa.


Na Israeli wote pamoja na wazee, viongozi wao na waamuzi wao, wakasimama upande huu wa sanduku na upande huu, mbele ya makuhani Walawi, waliolichukua sanduku la Agano la BWANA, huyo aliyekuwa mgeni pamoja na huyo mzalia; nusu yao mbele ya mlima Gerizimu, na nusu yao mbele ya mlima Ebali, kama Musa, mtumishi wa BWANA, alivyoamuru hapo awali, ili wawabariki watu wa Israeli.


kama vile Mungu Baba alivyotangulia kuwajua katika kutakaswa na Roho, hata mkapata kutii na kunyunyiziwa damu ya Yesu Kristo. Neema na amani na ziongezwe kwenu.


Neema, na rehema, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo Mwana wa Baba, zitakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo