Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Hesabu 19:11 - Swahili Revised Union Version

11 Mtu agusaye maiti yeyote atakuwa najisi muda wa siku saba;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

11 “Mtu akigusa maiti ya mtu yeyote, atakuwa najisi kwa siku saba.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

11 “Mtu akigusa maiti ya mtu yeyote, atakuwa najisi kwa siku saba.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

11 “Mtu akigusa maiti ya mtu yeyote, atakuwa najisi kwa siku saba.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

11 “Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote atakuwa najisi kwa siku saba.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

11 “Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote atakuwa najisi kwa siku saba.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

11 Mtu amgusaye maiti yeyote atakuwa najisi muda wa siku saba;

Tazama sura Nakili




Hesabu 19:11
22 Marejeleo ya Msalaba  

Nendeni zenu, nendeni zenu, tokeni huko, msiguse kitu kichafu; tokeni kati yake; iweni safi ninyi mnaochukua vyombo vya BWANA.


Hutangatanga njiani kama vipofu, Wametiwa unajisi kwa damu; Hata ikawa hakuna aliyeweza Kuyagusa mavazi yao.


Na kwa muda wa miezi saba, nyumba ya Israeli watakuwa wakiwazika, wapate kuitakasa nchi.


Naye akiisha kutakaswa watamhesabia siku saba.


Wanyama hao ndio walio najisi kwenu katika hao watambaao; yeyote atakayewagusa, wakiisha kuwa mgoza, atakuwa ni najisi hata jioni.


Kisha BWANA akamwambia Musa, Nena na hao makuhani, wana wa Haruni, uwaambie, Mtu asijinajisi kwa ajili ya wafu katika watu wake;


wala hataingia penye maiti, wala asijitie unajisi kwa ajili ya baba yake wala mama yake;


Mtu yeyote wa kizazi cha Haruni aliye na ukoma, au kisonono; asile katika vitu vitakatifu, hata atakapokuwa safi. Tena mtu yeyote atakayekinusa kitu kilicho na unajisi kwa sababu ya wafu, au mtu ambaye shahawa humtoka;


au kama mtu akigusa kitu kilicho najisi, iwe ni mzoga wa mnyama nyikani aliye najisi, au ni mzoga wa mnyama wa mfugo aliye najisi, au ni mzoga wa mdudu aliye najisi, bila kujua, akapata kuwa najisi, ndipo atakapochukua uovu wake;


Ndipo Hagai akasema, Kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti, akigusa kimojawapo cha vitu hivi, je, Kitakuwa najisi? Makuhani wakajibu, wakasema, Kitakuwa najisi.


Kisha mtu yeyote huko nje shambani atakayemgusa mtu aliyeuawa kwa upanga, au mzoga, au mfupa wa mtu, au kaburi, atakuwa najisi muda wa siku saba.


Nanyi fanyeni matuo yenu nje ya kambi muda wa siku saba; mtu yeyote aliyemwua mtu, na yeyote aliyemgusa mtu aliyeuawa, jitakaseni nafsi zenu siku ya tatu, na siku ya saba, ninyi na mateka yenu.


Waamrishe wana wa Israeli kwamba wamtoe kila mwenye ukoma kambini, na kila mtu aliye na kisonono, na kila aliye najisi kwa ajili ya maiti;


Siku hizo zote ambazo alijiweka awe wa BWANA asikaribie maiti.


Nena na wana wa Israeli, kuwaambia, Mtu wa kwenu, au wa vizazi vyenu, yeyote atakayekuwa na unajisi kwa ajili ya maiti, au akiwako mbali katika safari, na haya yote, ataishika Pasaka kwa BWANA;


Basi walikuwako wanaume kadhaa waliokuwa na unajisi kwa ajili ya maiti wa mtu, hata wasiweze kuishika Pasaka siku hiyo; nao wakaenda mbele ya Musa na Haruni, siku hiyo hao watu wakamwambia,


Ndipo Paulo akawatwaa wanaume wale, na kesho yake akajitakasa nafsi yake pamoja nao, akaingia ndani ya hekalu, akitangaza habari ya kutimiza siku za utakaso, hata sadaka itolewe kwa ajili ya kila mmoja wao.


Basi zile siku saba zilipokuwa karibu kutimia, Wayahudi waliotoka Asia wakamwona ndani ya hekalu, wakawataharakisha watu wote, wakamkamata,


Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi;


Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.


Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;


basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na dosari, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo