Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Hesabu 11:10 - Swahili Revised Union Version

10 Basi Musa akawasikia watu wakilia katika jamaa zao zote, kila mtu mlangoni pa hema yake; na hasira za BWANA zikawaka sana; Musa naye akakasirika.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Mose alisikia watu wakilia katika familia zote, kila mtu penye lango la hema lake. Basi, hasira ya Mwenyezi-Mungu iliwaka sana; naye Mose alichukizwa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Mose alisikia watu wakilia katika familia zote, kila mtu penye lango la hema lake. Basi, hasira ya Mwenyezi-Mungu iliwaka sana; naye Mose alichukizwa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Mose alisikia watu wakilia katika familia zote, kila mtu penye lango la hema lake. Basi, hasira ya Mwenyezi-Mungu iliwaka sana; naye Mose alichukizwa.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Musa akasikia watu wa kila jamaa wakilia, kila mmoja kwenye mlango wa hema lake. Mwenyezi Mungu akakasirika mno, naye Musa akafadhaika.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Musa akasikia watu wa kila jamaa wakilia, kila mmoja kwenye mlango wa hema lake. bwana akakasirika mno, naye Musa akafadhaika.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

10 Basi Musa akawasikia watu wakilia katika jamaa zao zote, kila mtu mlangoni pa hema yake; na hasira za BWANA zikawaka sana; Musa naye akakasirika.

Tazama sura Nakili




Hesabu 11:10
19 Marejeleo ya Msalaba  

Bali wakanung'unika hemani mwao, Wala hawakuisikiliza sauti ya BWANA.


Je! BWANA nisiwachukie wanaokuchukia? Nisiudhike nao watu wanaokuasi?


Hivyo BWANA aliposikia akaghadhibika; Moto ukawashwa juu ya Yakobo, Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli.


Mungu alisikia, akaghadhibika, Akamkataa Israeli kabisa.


Kwa sababu hiyo hasira ya BWANA imewaka juu ya watu wake, naye amenyosha mkono wake juu yao; akawapiga, navyo vilima vilitetemeka, na mizoga yao ilikuwa kama takataka katika njia kuu. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.


Nawe, naam, wewe nafsi yako, utaachana na urithi wako niliokupa; nami nitakulazimisha kuwatumikia adui zako katika nchi usiyoijua; maana umewasha moto katika hasira yangu, utakaowaka milele.


Kisha hao watu walikuwa kama wanung'unikao, wakinena maovu masikioni mwa BWANA; BWANA aliposikia hayo, hasira zake zikawaka; na moto wa BWANA ukawaka kati yao, ukateketeza hadi viunga vya kambi.


Musa akamwambia BWANA, Mbona umenitenda uovu mimi mtumishi wako? Kwa nini sikupata neema machoni pako, hata ukanitwika mzigo wa watu hawa wote juu yangu?


Umande ulipoiangukia kambi wakati wa usiku, hiyo mana ilianguka pamoja nao.


Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.


Hasira za BWANA zikawaka juu yao; kisha akaenda zake.


Basi wakaondoka hapo karibu na maskani ya Kora, na Dathani na Abiramu, pande zote; nao kina Dathani na Abiramu wakatoka nje wakasimama mlangoni mwa hema zao, pamoja na wake zao, na wana wao na watoto wao wadogo.


Watu wakamnung'unikia Mungu, na Musa, Mbona mmetupandisha huku kutoka nchi ya Misri, ili tufe jangwani? Maana hapana chakula, wala hapana maji, na roho zetu zinakinai chakula hiki dhaifu.


Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.


Akawakazia macho pande zote kwa hasira, akiona huzuni kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena.


Maana, moto umewashwa kwa hasira yangu, Unateketea hata chini ya kuzimu, Unakula dunia pamoja na mazao yake, Unaunguza misingi ya milima.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo