Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Amosi 5:13 - Swahili Revised Union Version

13 Kwa ajili ya hayo mwenye busara atanyamaza kimya wakati kama huo; kwa kuwa ni wakati mbaya.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

13 Basi, kutakuwa na wakati mbaya ambao hata mwenye busara atanyamaza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

13 Basi, kutakuwa na wakati mbaya ambao hata mwenye busara atanyamaza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

13 Basi, kutakuwa na wakati mbaya ambao hata mwenye busara atanyamaza.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

13 Kwa hiyo mtu mwenye busara hunyamaza nyakati kama hizo, kwa kuwa nyakati ni mbaya.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

13 Kwa hiyo mtu mwenye busara hunyamaza kimya nyakati kama hizo, kwa kuwa nyakati ni mbaya.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

13 Kwa ajili ya hayo mwenye busara atanyamaza kimya wakati kama huo; kwa kuwa ni wakati mbaya.

Tazama sura Nakili




Amosi 5:13
17 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini hao watu wakanyamaza kimya; wala hawakumjibu hata neno moja; maana amri ya mfalme ilikuwa kwamba, Msimjibu neno.


Na mimi, je! Ningoje, kwa sababu hawaneni, Kwa sababu wasimama kimya, wala wasijibu tena;


Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia, Ambaye hamna ubishi kinywani mwake.


Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;


Maana mwanadamu naye hajui wakati wake; kama samaki wanaokamatwa katika nyavu mbaya, na mfano wa ndege wanaonaswa mtegoni, kadhalika wanadamu hunaswa katika wakati mbaya, unapowaangukia kwa ghafla.


Lakini watu wakanyamaza kimya; wala hawakumjibu hata neno moja; maana ilikuwa amri ya mfalme, kwamba, Msimjibu neno.


Wakamwambia, Hezekia asema hivi, Siku hii ni siku ya dhiki, na aibu, na matukano; maana watoto wako tayari kuzaliwa, wala hapana nguvu za kuwazaa.


Lakini asishindane mtu, wala mtu asikemee; maana watu wako ni kama wao washindanao na kuhani.


Na mjomba wa mtu atakapomwinua, yaani, yeye amchomaye moto, ili atoe mifupa yake nyumbani, naye atakapomwambia yeye aliye katika pande za ndani za nyumba, Je! Yuko mtu yeyote pamoja nawe? Naye atakaposema, La, hapana; ndipo atasema, Nyamaza kimya; maana hatuna ruhusa kulitaja jina la BWANA.


Basi BWANA asema hivi, Angalia, nakusudia jambo baya juu ya jamaa hii, ambalo hamtazitoa shingo zenu, wala hamtakwenda kwa kiburi; kwa maana ni wakati mbaya.


Nikasikia, na tumbo langu likatetemeka, Midomo yangu ikatikisika kwa sauti ile; Ubovu ukaingia mifupani mwangu, Nikatetemeka katika mahali pangu; Ili nipate kuingoja ile siku ya dhiki, Kundi lao washambuliao wakweapo juu ya watu.


Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.


Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo